Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake
Tanzania (MEWATA), Dkt.Serafina Mkuwa (kulia), akitoa taarifa kwa
wanahabari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya uchunguzi na matibabu ya
Saratani ya Matiti na mlango wa kizazi mkoani Mwanza.
Kampeni hiyo itazinduliwa kesho katika
Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu
Hassan na baadaye kufanyika kwa siku mbili bure.
Na BMG
Kutoka kushoto ni Dkt.Mary Charles
ambaye ni Makamu wa Rais MEWATA, Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald
Subi, Rais wa MEWATI, Dkt.Serafina Mkuwa, Mwenyekiti Kamati ya Kampeni
na Mjumbe kamati tendaji MEWATA, Dkt.Magdalena Lyimo pamoja na Mratibu
wa huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoa wa Mwanza, Secilia Mrema.
Pia watumishi wa afya mkoani Mwanza
wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma za uchunguzi
wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi
0 comments:
Post a Comment