Jeneza lenye mwili wa Mbunge wa Dimani,
Zanzibar, marehemu Hafidh Ali Tahir, ukipandishwa kwenye ndege kwenye
uwanja wa ndege wa Dodoma, leo Novemba 11, 2016 kupelekwa kisiwani
Unguja kwa mazishi. Marehemu Hafidh ambaye alikuwa mjini Dodoma
akihudhuria vikao vya bunge, alifariki ghafla alfajiri ya leo Novemba
11, kwenye hospitali ya mkoa wa Dodoma alikokwenda yeye mwenyewe
kupatiwa matibabu baada ya kujsikia vibaya. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, aliwaongoza wabunge kuuaga mwili
wa marehemu kwenye jengo la bunge mjini Dodoma. Taarifa kutoka Zanzibar
zinasema, tayari mwili wa marehemu umewasili kisiwani Zanzibar na
mazishi yatafanyika baada ya sala ya Alasiri leo hii
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kwa mbunge wa Dimani,
Hafidh Ally Tahir kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Novemba 11, 2016.
Mbunge huyo alifariki dunia mjijini Dodoma usiku wa kuamkia leo. (PICHA
NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Spika
wa Bunge, Job Ndugai akitoa heshima za mwisho kwa mbunge wa Dimani, marehemu
Hafidh Ally Tahir kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Novemba 11, 2016
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai (wapili kushoto), Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Walemavu, Jenista
Mhagama (wakwanza kushoto) na Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Freeman Mbowe (wakwanza kulia) na wabunge wengine
wakisubiri kupokea mwili wa Mbunge wa Dimani, marehemu Hafidh Ally Tahir kwenye
viwanja vya bunge mjini Dodoma tayari kutoa heshima za mwisho
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa nasaha zake
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Mbunge wa
Dimai Hafidh Ally Tahir, bungeni mjini Dodoma Novemba 11, 2016
0 comments:
Post a Comment