Na
Theresia Mwami TEMESA Lindi
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania – TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu amepongeza
utaratibu unaotumika katika kituo cha TEMESA Lindi na karakana zake kwa
kuratibu vizuri kazi za kila siku.
“Nawapongeza
sana kwa utendaji wenu wa kazi kwa kuweka utaratibu wa kufuatilia kila kazi
inayofanywa na wafanyakazi wa kituo” alisema Dkt. Mgwatu.
Dkt
Mgwatu amemuagiza Meneja wa TEMESA Mkoa
wa Lindi Mhandisi Greyson Maleko kuhakikisha kuwa magari yote ya Serikali
mkoani Lindi yanafanyiwa matengenezo katika karakana ya TEMESA iliyopo mkoani
humo.
Dkt.
Mgwatu amemtaka Meneja huyo kuhakikisha anakusanya madeni yote wanayodai kwenye
Taasisi, Halmashauri na I
dara mbalimbali za Serikali kutokana na matengenezo ya
magari na mitambo, sambamba na kulipa madeni yote wanayodaiwa na wazabuni kwa
kipindi cha Julai-Septemba, 2016.
Kwa
upande wake Meneja wa TEMESA Lindi alisema kuwa changamoto kubwa inayokabili
kituo hicho ni uwepo wa madeni makubwa wanayodai kwenye Taasisi na Halmashauri
mbali mbali za serikali zilizopo Mkoani Lindi kutokana na matengenezo ya magari
na mitambo lakini wanajitaidi kuendelea kufanya kazi kwa ustadi na kujituma.
Katika
hatua nyingine Dkt. Mgwatu alitembelea eneo litakalojengwa gati kwa ajili ya
kivuko kutoka Lindi hadi Kitunda.
Dkt.
Mgwatu yupo katika ziara ya kikazi kutembelea mikoa ya Lindi na Mtwara ili
kujionea hali ya Vituo katika mikoa hiyo pamoja na utendaji kazi wake.
0 comments:
Post a Comment