Hivi
karibuni kumetokea na migongano ya kisheria na fitna ndani ya ngumi za kulipwa
na baadhi ya wavamizi kuitumia nafasi
hiyo kuisambaratisha kama sio kuua kabisa tasnia ya ngumi za kulipwa.kwa kujaribu
kufanya mapinduzi.
Ukweli ni kuwa kwa muda mrefu sana ngumi za
kulipwa hapa nchini zilikuwa zikiendeshwa na kuongozwa na makampuni hasa PST na TPBO huku TPBC nayo
ikijikokota kwa nyuma yao likisimamia jina bila kuwa na mapambano mengi ya
kueleweka. Huku mapambano yote makubwa na maubingwa yakisimamiwa na makampuni hayo na mawaziri
wenye dhamana husika wakiwa ndio wageni rasmi na kutoa michango yao, kwa
TPBO au PST au TPBC ltd, sasa iweje leo hawakubaliki?
Tukumbuke
TPBC ilikuja baada ya migogoro ya BUT ambao ni chama waanzilishi wa ngumi za kulipwa ndio maana
nikasema likisimamia jina lisipotee kwa kuwa hawakuwa wakifanya kazi zozote kwa
mda mrefu.
Baada ya
kuzaliwa tpbc hakukuwa na maendeleo mazuri kupelekea migogoro isiyokwisha na
kuzaliwa makampuni binafsi ya PST ,TPBO
na mengineyo ambayo ndio yaliyofufua tena ngumi za kulipwa na kuanza kupata umaarufu
na mabingwa tofauti na mabondia kupata mapambano mengi ya nje ambayo
yamewafanya mabondia wengi kujiajiri na kupata kipato cha kuwakwamua kupitia mchezo
huu wa ngumi. Ushindani nao wa mabondia ukaanza ongezeka ,ma gym ya ngumi
yanaongezeka nayo pia yakawa na ushindani na kuhakikisha wanajitahidi kutoa
mabondia wengi wazuri zaidi.
Mabondia
wakiwa wanaamini mapambano ya kimataifa ndio yana malipo mazuri kulinganisha na mapambano ya
kawaida ya ndani ya nchi hivyo kila bondia wa kulipwa alijitahidi acheze
mapambano mengi zaidi hata kwa gharama ndogo ili awe na rekodi itakayomwezesha
kupata mapambano yenye kiwango kizuri cha pesa .
Ngumi zikawa
zinapigwa viwango vinaongezeka kila bondia na mdau wa ngumi wakirudisha imani
kwa mchezo wa ngumi za kulipwa na mategemeo
makubwa zaidi kwa kiwango cha hali ya
juu.mambo yakawa yanakwenda raha mustarehe kuelekea kilele cha ubora duniani.
Kwa nia
njema ya kuendeleza huu mchezo usonge mbele na ufike hapo kileleni , makampuni
yote kwa pamoja yakaonelea yaanzishe umoja wao kwa ajili ya kupeana utaalamu na
kuwa na msemaji pindi itakapohitajika kuelezea muenendo wa ngumi,huku kila
kampuni ikiendelea na shughuli zake kama kawaida za ngumi ,
washirikiane
kwa pamoja kutanua wigo wa ushindi na mafanikio ya ndani na nje ya Tanzania,
Wakaonelea
katika umoja huo washirikishe mdau wa michezo toka serikalini maana nguvu
nyingi ishatumika kibinafsi na kwa kuupa heshima zaidi mchezo wa ngumi za kulipwa
, hapo wakapendekeza ,wawashirikishe baraza la michezo liwe karibu na ngumi za
kulipwa kwa lengo la kusaidiana kutatua matatizo na utaalamu.
wakitambua baraza la michezo linajishuhulisha zaidi na ngumi
za ridhaa.
na miaka ya hivi
karibuni ngumi za ridhaa zimekuwa haziendi vizuri zimedorola na kushindwa kufuzu kufanya vizuri katika mashindano mengi ,na ngumi za ridhaa zipo chini ya baraza la
michezo kupitia shirikisho lao la BFT ,
hivyo baraza lilitakiwa kuongeza umakini na BFT kuhakikisha
wanafanya vizuri , mabondia medali zinapatikana ,mabondia wanafuzu kushiriki
mashindano ya jumuiya ya madola ,
olyimpics na mashindano yote makubwa yanayohusiana
na ngumi za ridhaa, mikakati ya BMT bado haijaeleweka kuinusuru ngumi za
ridhaa.
na msingi mzuri wa ngumi za ridhaa(amacha) ndio unaoleta na kuzaa
mabondia wazuri sana wa ngumi kulipwa(professional boxers). Kukiwa na mabondia
wengi walioshiriki olyimpic na kadhalika ,wakijiunga na ngumi za kulipwa tayari
washakuwa mabondia wazuri na ni rahisi
kufundishwa kwa ajili ya maandalizi ya ubingwa hapo ni kazi ya makampuni na
mashirikisho ya kulipwa kumuendeleza
katika ajira yake hiyo (professional boxing) na kutuletea mataji.
Baraza la
michezo Tanzania(BMT) kupitia kaimu katibu wake bw Mohamed kiganja wakakubaliana na hilo la makampuni yote kuwa
na bodi na akawapa mamlaka ya kujichagua
viongozi wa muda na kutunga katiba ambayo ndiyo itakayoendesha haya makampuni
yote ya ngumi za kulipwa hapa nchini.
Akachaguliwa
bw habibu kinyogoli (KBF) kama
mwenyekiti.
Emmanuel
mlundwa (PST) katibu mkuu na chaulembo palasa(TPBC) kama katibu
msaidizi, Yasin Abdallah (TPBO) na Onesmo ngowi(TPBC ltd) kama wajumbe.
“hapa
ukiangalia mashirikisho yote makubwa ya ngumi za kulipwa Tanzania yamehusika “.MUENENDO HURU USIO NA UPENDELEO WOWOTE.
Wakajichagua
na kupendekeza jina la TANZANIA BOXING
AUTHORITY (TBA) .
Na katiba
itengenezwe mara moja watu wapige kazi.
wakiwa katika kipindi cha mchakato wa utengenezaji wa katiba kampuni ya
PST ikawa na skendo la uendeshaji wa
mchezo na kupelekea TPBC na TPBO
kuchochea kufungiwa huku, TPBC ltd ikitulia, TPBC na TPBO wakajichagua tena
uongozi mpya kutengeneza katiba ya TBA bila kuwashirikisha makampuni mengine.huku
msimamizi wa zoezi hilo bw kiganja kutolifuatilia.
Wakati
PST ikiwa katika mchakato wa rufaa na kupinga adhabu iliyopewa, katika
hali isiyo ya kawaida kaimu katibu mkuu
bmt Mohamed kiganja akateua kwa maneno TPBC kuwa ndie msimamizi mkuu wa ngumi za
kulipwa nchini bila kuwashirikisha makampuni mengine. Huku akisahau kuwa hapo
awali TPBC,TPBC LTD,PST,TPBO na makampuni mengine yote yalikuwa yakifanya kazi
zao sawa na muelekeo wa kufika kileleni(mafanikio)
,huku hao
tpbc wakiwa hawana nguvu sana wala wataalamu wa kutosha wa ngumi kulinganisha
na makampuni mengine. Wala uwezo wa kusimamamia mapambano makubwa ya ubingwa.
TPBC
walianza kulitumia vizuri rungu hilo
walilopewa na BMT kwa kuhakikisha mapambano yote yaliyo chini ya PST au TPBO
yanaharibika au wanasimamia wao .,jambo lililopelekea mapambano mengi kuvunjika
na mapambano waliolazimisha yakichezwa
kwa chini ya kiwango na nje ya malengo,
kwa mfano
tumeona likifanyika pambano kubwa la mamilion ambalo lilikuwa lisimamiwe kwa ushirika wa
tpbo na pst ambao wangewakilisha mikanda ya UBO na WBF ambayo dula mbabe alicheza na mchina, na
ibrahim class alikuwa acheze na bondia kutoka south afrika halikufanyika baada
yake south kukataa kucheza pambano
lisilo la ubingwa na kubadilishiwa mpinzani kiholela,
juu ya kutumika mamilion kuandaa na udhamini
ikashindikana kuchezwa ubingwa,na mapambano kadhaa wa kadhaa madogo yakishindwa
kuendeshwa ipasavyo, huku mapromota
wakiingia hasara na kuwa na manunguniko ya hapa na pale wakilalamika ngumi
zinapokwendea.
Jambo
lililoleta sintonfahamu katika tasnia ya ngumi za kulipwa ni pale TPBC
kulazimisha makampuni mengine ya ngumi na wadau wote wachukue vibali vya ngumi
kwao wao wakiwa kama ndio wakala wa serikali na wasimamizi wa ngumi za kulipwa
Tanzania kwa mamlaka waliyopeana na BMT kwa vigezo wanavyojua wenyewe pindi kuna
manunguniko ya rushwa na urafiki kuingizwa katika uteuzi huo. Kwa hiyo hapa
inaonekana kosa kubwa ni wadau wa ngumi
za kulipwa kujihusisha na bmt ambao
ngumi zinazowahusu kwa asilimia mia ni za ridhaa zinawashinda kuziendesha kila
leo mabondia wana hali ngumu sasa iweje leo wameshirikishwa kuuinua mchezo wa ngumi , wao wanageuza kitega uchumi na
kuingiza urafiki/undugu kupiga dili kupitia ngumi za kulipwa.
Hivi sasa
kumekuwa na maskendo ya hapa na pale katika tasnia ya ngumi za kulipwa huku
Tpbc wakizuia mabondia mapambano yao na kudiriki kuharibu hata safari za nje za
mabondia .misukosuko hii imepelekea kama bondia ukiwa karibu na kiongozi wa
kampuni Fulani ukicheza pambano hutopewa ushindi iwapo umeshinda . ni mambo yanayoongeza chuki na uhasama kati
ya viongozi wenyewe na mabondia pia kutokuwa na imani na mchezo wa ngumi.
Tpbc wakidai
wao ni wakala wa serikali kupitia BMT ,wamekuwa ni kero kwenye mzunguko mzima wa ngumi za
kulipwa kwa kukusanya pesa ambazo hazijulikani zinakwenda wapi . wamekuwa
wakikusanya pesa za matamasha ,vibali vya mapambano leseni nk. TPBC hailipi
kodi ikidai yenyewe ni bodi huku inaandaa mapambano yake na kusimamia maubingwa yake yenyewe ,ikizuia
wengine wasifanye kazi hizo kama si watu wao.
Wadau wa
mchezo wa ngumi kikubwa wanachojiuliza na wasiwasi wao kwa hao wahusika waliopo
huko tpbc wamepewaje mamlaka hayo makubwa bila kuhusishwa wadau wakuu wa mchezo
wenyewe,pia hao viongozi waliokuwepo
wameshawahi kutuhumiwa kujihusisha na biashara na usafirishaji wa madawa ya
kulevya na ofisi wamepewa ndani ya majengo ya serikali.pia wengine
walishajaribu kuuteka mchezo wa pooltable kwa njia kama hizihizi walizotekea
ngumi, kwanini huku kwenye ngumi wapewe majukumu wasiyoyajua kiutaalam wa
mchezo wawe wanahusika na safari za nje na ukusanyaji wapesa tu.tunajiuliza
hapa kuna namna!!?
Mapendekezo ya wanamasumbwi walio
wengi katika kuunusuru mchezo wa ngumi
hapa ulipo ni kuwa waitwe wadau wakuu na
makampuni yote yanayojihusisha na ngumi
za kulipwa mbele ya waziri mwenye dhamana husika akisimamia umaliziaji wa
utengenezaji wa katiba ya TANZANIA
BOXING AUTHORITY (TBA), ambayo itawajumuisha viongozi wote na wataalam wote
wangumi za kulipwa hiyo TBA ndio itakayokuwa ikisimamia uendeshaji wa ngumi
za kulipwa, UFANYIKE UCHAGUZI MWINGINE HURU WATAKAOSIMAMIA HIYO TANZANIA BOXING
AUTHORIY (bodi)
Sio kama ilivyo kwa sasa tpbc inajiita chama wakati
haina uchaguzi,na ndio waliojitwika
madaraka kupitia katibu mkuu BMT wakati wao ni kikundi kidogo cha wajanja
Fulani kinachofadhiliwa na mwanasiasa
mkongwe anayewania madaraka makubwa serikalini ,sasa tumekuwa wanamichezo ni
watu wa wakutumiwa kibiashara chafu za
madili na siasa.ofisi za TPBC zimehamia ndani ya ofisi za BMT tukiwa kama wadau
wa ngumi hatuelewi zinalipiwaje au kwa ufadhili gani?
Waziri
mwenye dhamana husika . okoa hili kabla halijaoza.
0 comments:
Post a Comment