Saturday, December 10, 2016


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akizungumza na waandishi wa habari akiwa na Mmiliki wa Kampuni ya kuzalisha saruji, DANGOTE kilichoko Mtwara, Alhaji Aliko Dangote, (katikati) na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam, Desemba 10, 2016.
NA K-VIS MEDIA
MMILIKI wa kiwanda cha kuzalisha saruji DANGOTE kilichoko Mtwara, Alhaji Aliko Dangote,  amevilaumu vyombo vya habari kwa uzushi kuwa anataka kufunga kiwanda chake na badala yake amesema, atawekeza zaidi hapa nchini na kwa kuhakikisha utayari wake,  ameagiza malori 600 ya kusambaza saruji na tayari batch ya kwanza ya malori hayoyamewasili bandarini.
"Kazi yetu hapa Tanzania ni kuja kuzalisha ajira hapa nchini, DANGOTE haina mpango wa kuingiza malighafi ya kuzalisha saruji au nishati kutoka nje, wakati vitu vyote hivyo vinapatikana hapa nchini." Alisema Dangote katika mazungumzo na waandishi wa habari ambapo Rais Magufuli alikuwepo. 
 Alhaji Dangote amemuhakikishia Rais Magufuli kuwa, uzalishaji wa saruji utaanza tena hivi karibuni baada ya marekebisho fulani yaliyokuwa yakifanywa kiwandani kukamilika.
 "Kama ni kweli ningekuwa nimetofautiana na serikali, nisingeweza kuagiza malori haya mapya kuja hapa nchini, na Rais nimemuhakikishia kuwa DANGOTE haikubaliani na kuingiza malighafi za kuzalisha saruji na badala yake tutasaidia viwanda hivyo vya kuzalisha malighafi ili kufikia lengo, kuingiza malighafi zinazopatikana hapa ni kuingiza umasikini na hilo halitawezekana, na nitaendelea kuwekeza hapa Tanzania, tumeshawekeza Dola milioni 600 kwenye kiwanda cha saruji na tutawekeza zaidi kwenye eneo la kilimo, asante sana Mhe. Rais." Alitoa hakikisho Mfanyabiashara huyo tajiri zaidi barani Afrika.
Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, amesema wataifuta kampuni ya Aqua baada ya kusababisha mtafaruku baina ya kiwanda cha DANGOTE, serikali na wananchi kwa kutaka "kupiga dili".
"Tatizo la watanzania ni watu hawa wa katikati, hapakuwa na taizo lakini pamekuwepo na watu wapiga dili kwenye mradi huu, badala ya DANGOTE kununua gesi moja kwa moja TPDC ambacho ni chombo cha serikali anaingia mtu katikati pale ili atengeneze kamisheni, tunataka eneo kwa ajili ya  JET, kaeneo kadogo tu watu wanataka zilipwe bilioni 43 kanakwamba watu wanachukua maeneo kule kusudi wakalipwe compensation, (fidia), kwahiyo wapiga dili ndio walikuwa wameingilia huu mradi kwahiyo wameshindwa na walegee." Alisema Rais Magufuli.
Rais pia alisema, " Walijiingiza wanasiasa, matapeli sijui na wanani, na wale sisi serikali tuta deal nao, kuna likampuni limejiingiza hapa katikati sijui linaitwa aqua, sijui nini, hili linafutiliwa mbali." Alisema Rais Magufuli. Kwa habari zaidi taarifa kamili ya Ikulu inapatikana hapo chini.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kumaliza kwa kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais akiagana na Alhaji Dangote


Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote akizungumza mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akizungumza na waandishi wa habari akiwa na Mmiliki wa Kampuni ya kuzalisha saruji, DANGOTE kilichoko Mtwara, Alhaji Aliko Dangote, (katikati) na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, (kulia) na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. (wakwanza kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Kapulya Musomba (wapili kushoto), baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam, Desemba 10, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao cha pamoja na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Sala
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu