Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na
Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurgenzi Mtendaji
wa Wakala wa Vyuo vya Nje ya Nchi (GEL) Bw. Abdulmalik Mollel (kulia)
alipotembelea banda la Wakala hiyo katika maonesho ya Viwanda vya Tanzania jana
Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Maendeleo ya
Biashara Tanzania (TANTARDE) Bw. Edwin Rutageruka
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akisikiliza
maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA)
Bw. James Ndege (watatu kutoka kushoto) alipotembelea maonesho ya Viwanda vya
Tanzania yaliyomalizika jana katika viwanja vya Mwl. Nyerere (sabasaba) Jijini
Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari na Elimu kwa Umma wa Mamlaka hiyo Bi.
Roberta Ferouz.
Baadhi ya wananchi wakipata huduma katika
banda la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) walipotembelea maonesho
ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko wa Shirika la Kuthibiti Viwango
Tanzania (TBS) Bi. Rhoda Mayugu akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda
lao katika maonesho ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na
Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akiangalia namna mashine ya kufyatulia matofali
inavyofanya kazi alipotembelea mmoja ya banda katika maonseho ya Viwanda vya
Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment