Tuesday, December 13, 2016

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurgenzi Mtendaji wa Wakala wa Vyuo vya Nje ya Nchi (GEL) Bw. Abdulmalik Mollel (kulia) alipotembelea banda la Wakala hiyo katika maonesho ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTARDE) Bw. Edwin Rutageruka
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Bw. James Ndege (watatu kutoka kushoto) alipotembelea maonesho ya Viwanda vya Tanzania yaliyomalizika jana katika viwanja vya Mwl. Nyerere (sabasaba) Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari na Elimu kwa Umma wa Mamlaka hiyo Bi. Roberta Ferouz.

 Baadhi ya wananchi wakipata huduma katika banda la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) walipotembelea maonesho ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.



 Afisa Masoko wa Shirika la Kuthibiti Viwango Tanzania (TBS) Bi. Rhoda Mayugu akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda lao katika maonesho ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.



 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Dkt. Adelhelm Meru akiangalia namna mashine ya kufyatulia matofali inavyofanya kazi alipotembelea mmoja ya banda katika maonseho ya Viwanda vya Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu