017
UWE MWAKA WA KULIPA KODI KWA HIARI.
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO
4.
January, 2017
MOJA ya malengo makuu ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuongeza
nguvu katika ukusanyaji wa mapato nchini kwa lengo la kupanua wigo katika
ukusanyanyi wa kodi ili kuimarisha mfumo wa utoaji huduma kwa wananchi.
Akifungua mkutano wa Bunge la 11 la Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania mwaka jana mjini Dodoma, Rais Dkt. John Pombe Magufuli alisema Serikali
yake itaongeza nguvu katika upanuzi wa wigo wa kodi na kuongeza ufanisi katika
ukusanyaji wa mapato.
Rais Magufuli alisema, Serikali yake itahakikisha kila mtu
anayestahili kulipa kodi analipa kodi stahiki kwa maendeleo ya nchi.
“Hatutasita kumchukulia hatua mtu yoyote atakayekwepa kulipa kodi,
tunawaomba wananchi mhakikishe mnapewa risiti kila mnaponunua bidhaa au huduma.
Kodi ni kitu muhimu kila mtu anayestahili kulipa kodi alipe” alifafanua Rais
Magufuli.
Aidha, alisema kuwa Serikali yake itahakikisha kila senti
inayoongezeka katika mapato ya Serikali inaelekezwa katika kutoa huduma bora
zaidi kwa wananchi na kuziba mianya ya upotevu wa fedha za Serikali ambayo inapunguzia
uwezo wa kuhudumia wananchi.
Taarifa ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inamtaka kila
Mfanyabiashara anayetumia mashine ya EFD anayekwepa kutoa risiti ni kosa la
kisheria ambapo adhabu yake ni kulipa faini isiyopungua sarafu ya pointi 100 hadi
pointi 150 ya thamani halisi ya fedha au kutumikia kifungo kwa kipindi
kisichozidi miaka mitatu au vyote kwa pamoja.
Aidha kwa mtu yeyote atakayeshindwa kudai au kutoa taarifa ya
kukataliwa kupewa risiti au ankara ya malipo ya bidhaa au huduma atakuwa
ametenda kosa na ikithibitika atatozwa faini isiyopungua sarafu ya pointi 2 na
zisizozidi sarafu ya pointi 100.
Hata hivyo kila
mfanyabiashara aliyesajiliwa na kodi ya Ongezeko la la Thamani anatakiwa
kuzingatia kutumia mashine za kodi za kielektroniki (EFD).
Hivyo basi Utii wa
Sheria bila shuruti katika masuala ya
kutoa na kudai risiti pindi tununuapo bidhaa ni jukumu letu sote na hivyo
kupelekea ongezeko la mapato kwa maendeleo ya Taifa letu.
Aidha dira ya Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) ni kuongeza mapato ya ndani kwa kuimarisha ulipaji wa
kodi kwa hiari, hivyo watanzania wenzangu tushirikiane na Mamlaka hiyo katika
kuongeza mapato ya ndani kwa maendeleo ya Taifa.
0 comments:
Post a Comment