NA K-VIS MEDIA/MASHIRIKA
YA HABARI
RAIS mteule wa Gambia,
Adama Barrow, ameapishwa leo kuwa rais wan chi hiyo leo Januari 19, 2017 kwenye
ubalozi wa Gambia ulioko nchi jirani ya Senegal.
Rais Barrow ameapishwa
na Rais wa Chama Cha Wanasheria cha Gambia,
Awali wasaidizi wakuu wa
Rais Yahya Jammeh wa Gambia, waanza kumkimbia, ikiwa ni saa chache kabla ya
Rais mteule wa nchi hiyo, Adama Barrow, kula kiapo jioni hii kwenye ubalozi wa
Gambia nchini Senegal.
Kiongozi wa juu kabisa
kumtoroka “Bosi” wake ni Makamu wa Rais, Isatou Njie Saidy na Mwanasheria wake Edu Gomez
.
Taarifa ya vyombo vya
habari vya kimataifa iliyotolewa leo Januari 19, 2018, inasema, vikosi vya
jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi, (ECOWAS), tayari vinajiandaa
kuivamia Gambia, ikiwa kiongozi huyo atang’ang’ania kuwa madarakani.
“Ikiwa Amiri Jeshi Mkuu
wa Gambia, atahitaji msaada wa kijeshi, majeshi ya ECOWAS yako tayari kufanya
hivyo,” Msemaji wa Serikali ya Nigeria aliiambia BBC.
Bw. Barrow ambaye
alishinda kiti cha Rais wa Gambia mwezi uliopita, amekimblia nchini Senegal kwa
usalama wake, na ameandika katika akaunti yake ya Tweete akisema, ataapishwa
leo Alhamisi Januari 19, 2017 kwenye ubalozi wa Gambia nchini Senegal.
Vikosi vya ECOWAS vikiongozwa na Senegal tayari
viko mpakani vikisubiri amri kuvuka mpaka.
Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Gambia, Sidi
Sanneh, amesema, kuna mgawanyiko katika jeshi la Gambia, wakati Mmkuu wa
Majeshi tayari ameshatangaza kuwa vikosi vyake havitajiingiza katika vita ya
kijinga, lakini kuna kundi dogo la wanajeshi linalofaidi zaidi linaweza kuleta
upinzani.
Rais Yahya Jammeh, akiwa na umri wa miaka 29
mwenye cheo cha Luteni, aliongoza kikundi cha wanajeshi na kumpindua Rais
aliyekuwa madarakani wakati huo, Dawda Jawara, Julai 22, 1994. Mapinduzi hayo
hayakuwa na umwagaji damu.
Naye Dawda Jawara aliitawala nchi hiyo tangu
mwaka 1970.
0 comments:
Post a Comment