NA K-VIS
MEDIA/Khalfan Said
TRENI ya mwendo
haraka, (DELUX), iliyokuwa ikitokea Kigoma kuja jijini Dar es Salaam,
imeanguka eneo la Ruvu mkoani Pwani jioni hii ya Januari 29, 2017.
Kwa
mujibu wa
taarifa zilizopatikana kutoka eneo la ajali,zinasema takriban mabehewa
10 yameanguka na juhudi za kuwaokoa watu zilikuwa zikiendelea na watu
kadhaa walionekana wakiwa wamelala chini wengine hawajiwezi kabisa.
Msemaji wa TRL,
Medladjy Maez amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na alipoongea na mwandishi wa
habari hizi majira ya saa 11;13 jioni, amesema treni hiyo imeanguka na ni
mabehewa matano ya abiria yameanguka na moja limeacha njia, lakini hakuwa na
taarifa zaidi kwani ndio alikuwa anajiandaa kuelekea eneo la tukio.
“Ni kweli treni
yetu ya Delux iliyokuwa ikitokea Kigoma na kutarajiwa kuwasili hapa saa 11:30,
imeanguka eneo la Ruvu, na mabehewa matano yameanguka na moja limeacha njia,
taarifa zaidi tutazitoa kuhusu walioathirika kwa sasa tunajiandaa kwenda eneo
la tukio” Alisema Maez.
Habari mpya zilizotufikia kutoka kwa
msemaji wa TRL, Midladjy, zinasema treni hiyo imeanguka majira ya saa
9:40 alasiri. "Treni yetu ya Deluxe ilipokuwa ikirejea Dar kutoka Kigoma
imepata ajali kati ya vituo vya Ruvu na Ngeta ambapo mabehewa 9
yamepata ajali . Kati ya hayo manne yameanguka, mawili yametenguka na
matatu yameacha njia..Imeripotiwa watu kadhaa wamepata majeraha mepesi
isipokuwa mmoja ndiye aliyepata majeraha makubwa.amekimbizwa hospitali
kwa matibabu zaidi. Hizi ni taarifa za awali..baada ya Kikosi cha
uokoaji kikimaliza kazi ya kuinua mabehewa ndio taarifa ya Wahanga
itakamilika! Wakati taarifa hii ikipatikana Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa. .Mkuu wa TRL Ndugu Kagosa
Kamanda Kikosi cha Polisi Reli Mhandisi Chillery wako njia kuelekea
katika eneo la ajali! . Sehemu ya treni ya Deluxe yenye mabehewa kumi
iko njiani kuja Dar es Salaam inatarajiwa kufika saa 2 usiku huyu.,
amesema Bwana Maez.
Abiria na wasamaria wakiokoa abiria
kutoka treni ya mwendo haraka ya Delux iliyokuwa ikitoka Kigoma kuja
jijini Dar ES Salaam, baada ya kuanguka eneo la Ruvu mkoani Pwani jioni
hii ya Januari 29, 2017.
0 comments:
Post a Comment