|
Rais Msataafu wa Awamu
ya Tatu wa Tanzania, Benjamin William Mkapa akizungumza mara baada ya kupokea
Matembezi kwa ajili ya kupinga ujangili ya Walk
for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya
kilomita tano yameratibiwa na Asasi ya Tanzania – China Promotion Association (TCFPA)
na Ubolozi wa China ambapo yalianzia ubalozini na kuishia katika Hotel ya Sea
Cliff.
|
|
Balozi wa China nchini
Dkt. Lu Youqing, akizungumza kabla ya kuanza matembezi ya Walk
for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya
kilomita tano yana lengo la kuhamasisha upingaji wa ujangili na mauaji ya
Tembo.
|
|
Katibu Mkuu wa Asasi ya
Tanzania – China Promotion Association (TCFPA) Joseph Kahama akitoa maelekezo kuhusu matembezi
ya Walk
for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya
kilomita tano yameratibiwa na asasi hiyo kwa kushirikiana na Ubolozi wa China
ambapo yalianzia Ofisi za Ubalozi wa China na kuishia katika Hotel ya Sea
Cliff.
|
|
Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni Ally Hapi (kushoto) akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Dkt.
Lu Youqing wakati wa matembezi ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017
yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Lengo la matembezi hayo ni kuhamasisha
jamii kupinga ujangili na mauaji ya Tembo.
|
|
Balozi wa China nchini
Dkt. Lu Youqing, akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kufanya
mazoezi kabla ya kuanza matembezi ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo
jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yana lengo la kuhamasisha
upingaji wa ujangili na mauaji ya Tembo.
|
|
Balozi wa China nchini
Dkt. Lu Youqing (mwenye tisheti nyekundu), akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji
la Dar es Salaam katika matembezi ya
Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya
Maliasili na Utalii Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi na kulia kwa Balozi
ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi.
|
|
Baadhi ya washiriki wa
matembezi ya Walkt for Elephant Dar es Salaam 2017 wakiwa wakionyesha umoja wao
katika kupinga mauaji ya Tembo mara baada ya kufika katika viwanja vya Hoteli
ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam leo.
|
|
Wanamuziki Mrisho Mpoto
na Banana Zoro wakiimba wimbo wenye ujumbe kuhusumauaji ya Tembo mbele ya Rais
Mstaafu Benjamini Mkapa wakati wa hafla ya matembezi ya Walk for Elephant Dar
es Salaam 2017 yaliyofanyika leo.
Picha zote na: Frank Shija
|
Na Daudi Manongi
Katibu Mkuu
Wizara ya Maliasili na Utalii Meja.Gen Gaudence Milanzi amewaasa wafugaji
kuacha kuingiza mifugo katika hifadhi za taifa ili kuzitunza hifadhi hizo.
Katibu Mkuu
uyo aitoa wito huo wakati akizungumza baada ya kufanya matembezi ya kupinga ujangili
unaofanywa dhidi ya Tembo
ya kilometa 5 kutoka Ubalozi wa China
mpaka Hoteli ya Sea Cliff ambapo wageni
mashughuli kama Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe.Benjamini William Mkapa
alishiriki.
“Hifadhi za taifa hapa nchini hazina budi kulindwa na
kutunzwa ili vizazi vijavyo viweze kuzifaidi kwani maeneo hayo yametengwa kwa ajili ya wanyama pori pekee na
siyo kwa mifugo na hivyo kila mwananchi analo jukumu la kuyalinda mazingira
haya,”Aliongeza Mej.Gen Milanzi.
Awali akizungumza katibu mkuu huyo alisema kuwa Serikali ina
mkakati mkubwa wa kuhakikisha inashirikiana na nchi zingine katika kutokomeza
kabisa Ujangili wa pembe za ndovu nchini.
Aidha aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa
kuwa mstari wa mbele katika kupambana na ujangili wa pembe za ndovu ikiwemo
upigaji marufuku
biashara ya pembe za ndovu na viwanda vya kuchonga pembe hizo ifikapo
mwezi machi Mwaka huu.
Mbali na hayo katibu Mkuu uyo amewaasa watanzania kuwafichua
wale wote wanaojihusisha na biashara hiyo na kuonya kuwa kwa kushiriki katika
biashara hii tutawafanya tembo wetu kuwa historia kwani hawatakuwepo tena.
Naye Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe.Benjamini William Mkapa amewataka
watanzania kulinda na kutunza mbuga zetu kwani ni urithi wa kila mtanzania na
kuzitaka nchi mbalimbali kusaidia katika kulinda urithi huu wa wanyama na
kuvitaka vyombo vya habari kushiriki vyema katika kutangaza mbuga zetu na pia
kutangaza jitihada zinazofanywa na serikali katika kutokomeza ujangili wa pembe
za ndovu.
0 comments:
Post a Comment