Miji Sita ya Zanzibar Kufanyiwa Mipango ya
Matumizi ya Ardhi Ifikapo 2020
Na.
Lilian Lundo – MAELEZO.
03/01/2017
SERIKALI ya Mapinduzi
Zanzibar (SMZ) inatarajia kukamilisha upangwaji wa matumizi ya ardhi kwa ajili
ya maboresho ya Miji Sita ifikapo 2020.
Hayo yamebainishwa na
Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Mhe. Salama Aboud Talib katika
mahojiano na mwandishi wa habari hii kuhusu mafanikio ya Mkakati wa Matumizi ya
Ardhi Zanzibar wa mwaka 2015.
Mhe. Salama amesema
kuwa kumekuwa na mafanikio makubwa katika sekta ya ardhi mara baada ya kuanzishwa kwa Idara ya
Mipango Miji na Vijiji ambayo ilipelekea kuanzishwa kwa mpango mkuu wa matumizi ya Ardhi uliosaidia
kwenda kasi kwa shughuli za upangaji wa
matumizi ya ardhi ukilinganisha na miaka ya nyuma.
“Malengo ya Awamu ya
Saba katika kupanga Miji ni kutengeneza mipango ya matumizi ya Ardhi (Master
Plan) ya miji Mikuu miwili ambayo ni Zanzibar na Mji wa Chake-Chake na kufanya
Mipango ya Maendeleo (Local Area Plan) ya miji midogo 14,” alifafanua Mhe.
Salama.
Aliongeza kuwa kati
ya miji Mikuu miwili, Mji wa Zanzibar umeshafanyiwa mipango ya matumizi ya
ardhi na kati ya Miji 14, Miji 3 ya Nungwi, Chwaka na Mkokotoni imeshafanyiwa
mipango yake.
Aidha amesema kuwa
hadi kufikia mwaka 2020, Miji 6 itakuwa imefanyiwa mpango wa matumizi ya Ardhi.
Aliitaja Miji hiyo kuwa ni Chake-Chake, Wete, Mkoa, Mkunduchi, Dunga na Mahonda.
Mhe. Salama amesema
kuwa tangu mwaka 1964 ni awamu hii ya
saba ndiyo inayotoa kipaumbele katika masuala ya miji, ambapo taasisi maalum ya
masuala ya miji imeundwa.
Pia kumekuwa na
utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ya mwaka 1968 ambayo imepata nguvu
tena kwa kurudisha dhana adhimu iliyotungwa baada ya Mapinduzi ya kuwa na
kitovu cha mji “Ngambo Tuitakayo”.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment