RBA YAANDAA
MASHINDANO MPIRA WA KIKAPU.
NA BEATRICE
LYIMO-MAELEZO
10/01/2017
Chama cha mpira wa
Kikapu Dar es salaam (RBA) kimeanzaa mashindano ya ligi ya mpira huo yatakayoshirikisha
timu 16 kutoka kwa wananume na timu nane za wanawake.
Akizungumza na
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa chama hicho Okare
Emesu alisema kuwa ligi hiyo inatarajiwa kuanza Januari 28 mpaka julai 30 mwaka huu.
Alisema kuwa viongozi
wa RBA wamekuja na mikakati hiyo ili kuleta chachu kwenye maeneo mengine ya mkoa,
ligi ya watoto chini ya miaka 14, ligi ya daraja la kwanza, ligi ya vyuo, ligi
ya mashirika, ligi ya mashule, program maalumu kwa ajili ya kukuza vipaji kwa
mpira wa kikapu nchini.
“Tangu kuanzishwa kwa
chama hiki, kumekuwa na mafanikio ya muda mfupi ikiwemo ushiriki kwenye
mashindano ya Taifa na kushika nafasi ya pili kwa wanaume na wanawake jambo
ambalo halikuweza kufanyika kwa takribani miaka mitatu sasa” Alisema Mwenyekiti
huyo.
Aidha akizungumzia
kuhusu mfumo wa ligi utakaotumika kwenye mashindano hayo, Mkurugenzi wa
Mawasiliano na Masoko RBA Peter Mpangala alisema kuwa mfumo utakaotumika ni
mfumo wa nyumbani na ugenini katika hatua za awali na timu nane za wananume za
nafasi za juu zitacheza mtoano hadi kupata bingwa.
Mbali na hayo alisema
kuwa kutakuwa na maonyesho ya awali ya ligi ya RBA (Pre RBA Show case) siku ya
Mapinduzi januari 12, mwaka huu kwenye viwanja vya mpira wa kikapu vya Gymkhana
yakilenga kukaribisha wadau mbalinmbali kuona mfano wa ligi ya RBA
itakavyokuwa.
Timu zinazotarajiwa
kushiriki kwenye ligi hiyo kwa upande wa wanaume ni JKT, Mgulani, Ukonga Kings,
Magereza, Savio, Pazi, DB Youngstars, Magnet, ABC, Mabibo Bullets, Outsiders,
Kurasini heat, Oilers, Vijana, Chui na Jogoo na kwa upande wa wanawake ni JKT
Stars Jeshi Stars, Vijana Queens,
DonBosco Lioness, Ukonga Queens, Kurasini Divas na Oilers Princess.
0 comments:
Post a Comment