Friday, January 27, 2017

Waziri mkuu Mhe Majaliwa asema wanaojichomeka eneo la mgodi ili wapate Fidia kutolipwa


 Waziri mkuu wa tanzania Mhe. Kassm Majaliwa (Katikati) akizungumza na baadhi ya viongozi mkoani Njombe katika eneo la Liganga nyuma yake ni Mawe yanayo daiwa kuwa na Chuma Cha liganga
 Waziri Mkuu Wa Tanzania Kassm Majaliwa Akizungumza na wakazi wa Ludewa Mkoani Njombe ambako anatoa onyo wa wanao jifanya wananchi na kuvamia migodi la Liganga
 Ngomba ya Kinyakyusa ikimpokea waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa katika viwanya vya shule ya mpira Ludewa Mjini ambako amezingunza na wananchi
SERIKALI imesema kuwa itahakikisha kuwa wananchi wanao zunguka mradi wa Machimbo ya Liganga machimbo ya chuma ambao unatarajia kuanza hivi karibuni ambapo kunatarajiwa wananchi hao kulipwa na kuanza Machimbo katika eneo hilo ambapo onyo kwa wale ambao wameanza kuanza kujichomeka na kupata fidia.

Waziri Mkuu ametembelea eneo la machimbo ya Liganga wilayani Ludewa ambapo mbunge wa jimbo la Ludewa anaomba kwa waziri wananchi wake kulipwa fidia na kuwekwa kwa lami barabara ya kutoka Mkiu kuingia mpaka katika mladi wa Liganga.

Waziri akielekea wilayani ludewa anakutana na wananchi wanao msimamisha katika kijiji cha Lusitu ambapo wananchi wanamfikishia kilio chao kwa kutumia nyimbo.

Kabla ya kuingia ludewa mjini waziri anaingia Liganga ambako chuma litachimbwa kwenye mlima wa mawe ya chuma lenye ukubwa wa kilomita kumi ambapo akiwa hapa anazungumza na viongozi wa mkoa wa Njombe.

Baada ya kumaliza kutembelea mradi huu waziri mkuu anakutanan ana wananchi ambapo suala ya fidia mbunge analisema mele ya mkutano wa hadhana huku barabara nayo ikiombwa kuwa ya lami kutoka Mkiu hadi Liganga.

Na haya ndio majibu ya waziri mkuu huhusu umeme, fidia na huduma zinginde za za kijamii.
Kuhusu kukamilika  kwa kulipa fidia na kuanza kwa mradio huo waziri anaongeza.

Baada ya kutoka eneo la mgodiwaziri mkuu anaelekea mjini  Ludewa kwaajili ya Mkutano wa Hadhara   na kuzungumza na wakazi wa  mjini Ludewa ambapo suala la maji na barabara linaibuka tena.


--
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu