Meya
wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Mwita,akizungumza na wajumbe wa baraza la
madiwani wa jiji hilo katika Ukumbi wa Karimjee leo,wakati wa kupitisha makisio
ya bajeti ya matumizi ya ndani ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2016-17
yenye jumla ya Sh.Bilioni13.177 ambayo ni sawa na asilimia 72%. Kulia ni
Mkurugenzi wa Jiji hilo,Sipora Liana na Naibu Meya wa Jiji,Mussa Kafana. (PICHA ZOTE NA ELISA SHUNDA)
NA ELISA SHUNDA
BARAZA la
Madiwani Jiji la Dar es salaam limepitisha kwa kauli moja makisio ya bajeti ya
matumizi ya ndani ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2016-17 yenye jumla ya
Sh.Bilioni13.177 ambayo ni sawa na asilimia 72%.
Akisoma taarifa
hiyo mbele ya baraza hilo,Mkurugenzi wa Jiji,Sipora Liana alisema kuwa fedha
hizo zinatokana na mapato ya vyanzo vya ndani ambapo ni makisio ya bajeti
kuanzia mwaka 2015/2016 ya utendaji kazi wa halmashauri ya jiji kwa miaka hiyo
na mpango kazi kwa bajeti ya mwaka 2016/2017.
Aidha
Liana amefafanua kuwa jumla ya makadirio ya mwaka wa fedha 2015/16 ni
Sh.Milioni 13.177 ambapo Sh.Milioni 5.403 ni ruzuku kutoka serikali kuu huku
Sh.Milioni 7.167 ni fedha zinatokana na vyanzo vya mapato ya ndani na salio
anzia ni Sh.Milioni 332.135,katika kipindi cha Julai 2015 mpaka Juni 2016 kiasi
cha Sh.Milioni 9.508 kilikusanywa ambacho ni sawa na asilimia 72.16 ya jumla ya
bajeti.
''jumla ya Sh.Milioni 668.403 zitatumika kuwalipa watumishi wa jiji la Dar es salaam huku Sh.Milioni 4.518 fedha za miradi ya maendeleo ambapo jumla ya fedha 2.312 zilizotolewa na serikali kuu zinatarajiwa kuwalipa watumishi wa serikali ''Alisema Liana.
Alisema
kuwa katika kipindi cha mwaka 2016/17 makisio ya bajeti katika jiji hilo yalikuwa
ni Sh.Milioni 11.352 ambapo kati ya Sh. 3,595 ni ruzuku kutoka serikali na
jumla ya Sh. 7.756 ambazo zimetokana na makusanyo ya kodi mbalimbali kama
mapato ya ndani sawa na asilimia 60.53 ya bajeti yote .
Alisema kati ya Sh. Milioni 50 katika bajeti hiyo ziliweza kutumika katika kufanya tahimini na ukaguzi wa miradi mbalimbali ya jiji hilo huku Sh. Milioni 20 zilitumika katika kuandaa mikakati ya jiji hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo .
Naye Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Mwita,amewataka madiwani wa baraza hilo la Jiji kuwatumikia wananchi na kuziheshimu nafasi zao kwani kwa sasa wananchi wanataka maendeleo kwa kasi na kuangalia kero mbalimbali zinazolikabili jiji hilo na kuacha ushabiki wa kisiasa ambao utaleta mkwamo wa maendeleo.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ubungo,Saed Kubenea alilitaka baraza hilo
kutenga bajeti ya kuboresha huduma mbalimbali za jamii katika jiji hilo ikiwemo
zahanati na kutaka madiwani wa kata hiyo kuwa na akidi ya wajumbe
inayojitosheleza katika mikutano yake inapoamua kupitisha mambo ya msingi kama
hayo.
Diwani wa Kata ya Tabata,Patrick Assenga (Chadema) akichangia katika kikao cha bajeti hiyo. |
Mbunge
wa Temeke,Abdallah Mtolea,akichangia mada wakati wa kiako hicho cha baraza la
madiwani wa halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Mbunge
wa Jimbo la Ubungo,Saed Kubenea (Chadema),akifuarhia jambo na Mbunge wa Jimbo
la Kigamboni,Dk.Faustine Ndugulile (CCM) wakati wa kikao cha baraza la madiwani
wa Jiji la Dar es Salaam kujadili na kupitisha bajeti ya mwaka 2016/17 ya jiji
hilo katika Ukumbi wa Karimjee
0 comments:
Post a Comment