Sunday, February 5, 2017

SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI ATEMBELEA MOI


Daktari Bingwa Upasuaji wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu MOI, Nicephorus Rutabasibwa (kulia) akifafanua jambo kwa Spika wa Bunge Job Ndugai  (wa tatu kushoto) Dar es Salaam jana wakati alipofika kumjulia hali Mkurugenzi Msaidizi wa Tehama (ICT)  wa Bunge, Lily Mraba aliyelazwa katika Taasisi hiyo
 Muuguzi Mwandamizi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI), Zaituni Bembe (kushoto) akiagana na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai  Dar es Salaam jana mara baada ya kutoka katika Taasisi hiyo, wakati alipokwenda kumjulia hali Mkurugenzi Msaidizi wa Tehama (ICT) wa Bunge, Lily Mraba.
Daktari wa Mishipa ya Fahamu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI)  Hamisi Kinyerero akiagana na maofisa wa Bunge walioongozana na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai wakati alipofika kumjulia hali Mkurugenzi Msaidizi wa Tehama (ICT) wa Bunge, Lily Mraba. aliyelazwa katika Taasisi ya Mifupa MOI. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA )
iv dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu