Saturday, March 11, 2017

 MWENYEKITI wa CCM, Rais John Pombe Magufuli, (pichani wapili kushoto), akiongoza kikao cha Kamati Kuu (CC), ya chama hicho kwenye ukumbi wa Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma almaarufu kama White House, leo Machi 11, 2017. Katika kikao hicho, viongozi wengine wa juu wa CCM waliohudhuria ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM, (Zanzibar), Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM, (Bara), Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Makamu wa Rais, Samia Sukluhu Hassan, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Ali Seif Iddi, Spika wa Bunge, Job Ndugai, Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zuberi Ali Maulid. Kikao hicho kitafuatiwa na kile cha Halmashauri Kuu, (NEC), kabla ya Mkutano Mkuu Maalum utakaoanza kesho Jumapili Machi 12, 2017, ambao jukumu lake kubwa ni kupitisha mabadiliko ya katiba ya chama hicho ya mwaka 1977 pamoja na kanuni zake.

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa utangulizi kumpa nafasi Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk JohnMagufulikufungua na kuongoza kikaocha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma. Kushoto ni Dk. Shein na Kulia ni Mangula.
   Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo na Shamsi Vuai Nahodha wakibadilishana mawazo kabla ya kikao hicho kuanza leo mjini Dodoma.

  Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo na Shamsi Vuai Nahodha wakibadilishana mawazo kabla ya kikao hicho kuanza leo mjini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akisalimiana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulidikabla ya kuanza kikao hicho. Katikati ni Spika wa Bunge Job Ndugai
  Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kikao hicho. Kushoto ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni Mohamed Seif Khatib na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai
Mwenyekiti wa CCM, Rais John Pombe Magufuli, akipokewa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana, (kushoto), wakati akiwasili makao makuu ya chama hicho kuongoza kikao cha Kamati Kuu na kile cha Halmashauri Kuu mjini Dodoma Machi 11, 2017. (PICHA NA BASHIR NKOROMO)
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu