Na Anitha Jonas – WHUSM
13/12/2017
Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Dkt.Harrison Mwakyembe amewataka
wachezaji wa Timu ya Stand United
kuchukua Kombe la Ligi Kuu .
Mheshimiwa Mwakyembe ametoa kauli hiyo alipokuwa
katika mkutano wa kutangazwa kwa mdhamini wa timu hiyo ambaye ni BIKOSPORTS aliyetoa udhamini wa Sh. Milioni Mia Moja
pamoja na kununua jezi za wachezaji watakazo tumia katika msimu huu wa ligi.
“Soka la leo siyo kama la zamani linahitaji uwekezaji
na pesa za kutosha kusaidia kupata
wachezaji wazuri wenye viwango vya juu,Makocha wenye uweledi na mazingira mazuri ya kufanyia mazoezi kwa
wachezaji,”Mhe.Dkt. Mwakyembe.
Naye Mweyekiti wa Timu ya Stand United Bw.Dkt.
Ellyson Maeja alitoa shukrani kwa Kampuni ya Biko kwa udhamini huo na kuaahidi kutumia fedha hizo vizuri kwa
manufaa ya timu ikiwa ni pamoja kulipa
mishahara ya wachezaji.
“Tunashukuru sana Biko kwa udhamini huu pia
napenda kuwa hahikisha kuwa fedha hizi zitatumika vizuri pamoja na kuongeza
chachu katika maendeleo ya timu ikiwemo kujituma kwa wachezaji wa timu na
kuleta mafanikio makubwa katika msimu huu wa ligi,”Dkt.Mgeta.
Pamoja na hayo naye Mkurugenzi Mtendaji wa BIKO
Bw.Charles Mgeta alitoa wito kwa
makampuni mbalimbali kujitokeza na kusaidia sekta ya michezo nchini kwa
maendeleo ya taifa letu pia amewataka watanzania kuendelea kucheza bahati
nasibu ya BIKOSPORTS sababu ni rahisi na unalipwa kwa haraka.
*****************MWISHO*********************
0 comments:
Post a Comment