Wednesday, February 21, 2018

DAWASA NA DAWASCO ZATAKIWA KUPELEKA HUDUMA ZA MAJI PEMBEZONI MWA JIJI LA DAR

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Juma Aweso (wa pili toka kulia) akiwa na katibu tawala wa Wilaya ya Temeke, Edward Mpogolo wakati wakipatiwa maelezo machache juu ya uharibifu wa miundo mbinu ya maji inayofanywa na wananchi wasio waaminifu wakati wa ziara ya Naibu huyo aliyoifanya katika manispaa ya Temeke na Ilala ili kujionea miradi mbali mbali ya maji.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Juma Aweso akiangalia moja ya mradi wa maji.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Juma Aweso amezitaka mamlaka zinazohusika na usambazaji wa huduma ya maji safi na taka (DAWASA na DAWASCO) kuendelea kusambaza huduma pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Kauli hiyo ameitoa Februari 19, 2018 jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake aliyoifanya katika manispaa ya Temeke na Ilala ili kuweza kujionea miradi mbali mbali iliyoanzishwa ili kuweza kuwafikia huduma ya maji kwa urahisi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu