Saturday, March 17, 2018

BENKI YA CRDB YAJITOSA KUKISAIDIA CHAMA CHA MAAFISA HABARI,MAWASILIANO NA UHUSIANO SERIKALINI (TAGCO).
Meneja Uhusiao wa Benki ya CRDB,Godwin Semunyu akizungumza mara baada ya kuwasilisha mada wakati wa Mkutano Mkuu wa 14 wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa (AICC) jijini Arusha.
Meneja Uhusiao wa Benki ya CRDB,Godwin Semunyu akiwasilisha mada wakati wa Mkutano Mkuu wa 14 wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa (AICC) jijini Arusha.
Washiriki wa Mkutano Mkuu wa 14  wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB ,Godwin Semunyu wakati wa mkutano huo. kutoka kulia ni Mwenyekiti wa TAGCO,Pascal Shelutete,Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Laurean Bwanakunu na mwisho kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Sanaa,Utamadunina Michezo,Susan Mlawa.
 Baadhi ya Washiriki wa Mkutano huo.
 Meneja Uhusiao wa Benki ya CRDB,Godwin Semunyu akiwasilisha mada juu ya mfumo maalumu wa kadi za kielektroniki maarufu kama Credit Card ,huduma ambayo inatolewaa na Benki ya CRDB.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano mkuu wa 14 wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Meneja Uhusiao wa Benki ya CRDB,Godwin Semunyu .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini .

BENKI ya CRDB imeahidi  kuendelea kukisaidia Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikali na kwamba kufanya hivyo kutasaidia upatikanaji wa taarifa zilizo sahihi na kwa wakati sahihi.

Hayo yameelezwa na Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB,Godwin Semunyu wakati akiwasilisha mada wakati wa kikao kazi cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa (AICC) jijini Arusha ,sambamba na mkutano mkuu wa chama hicho (TAGCO) 

"Benki ya CRDB tunaamini "with right information" ambao hawa ni haki yao kuifikisha kwa wananchi ambao watakuwa aware nini kinaendelea,sio tu katika kutangaza nafasi za kazi kama baadhi ya watu wanavyofikiria ,pia wanahusika katika kutangaza Zabuni  zilizopo,nafasi za Maendeleo,Nafasi za uwekezaji na sSehemu gani hasa unaweza kuwekeza kwa ajili ya maendeleo."alisema Semunyu.

Amesema Maafisa Habari wa taasisi za Serikali ndio daraja la kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi na kwamba kupitia kwao kila kinachofanyika ndani ya Serikali kitwafikia wananchi kwa njia na wakati sahihi.

"Kama alivyosema Msemaji Mkuu wa Serikali kwamba kuna tofaui kubwa ya kufikisha habari na kufikisha habari sahihi,kwa hiyo daraja hilo ambalo kwa muda mrefu limekuwa halipati heshima stahiki sasa litapa heshima."alisema Semunyu.

Mwisho 

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu