Sunday, December 30, 2012

MIKOCHENI CITY YATWAA KOMBE LA DIWANI


Meya wa Manispaa ya Kinondoni na Diwani wa Kata ya Mikocheni, Yusuf Mwenda akikabidhi kombe la Diwani kwa Nahodha wa timu ya Mikocheni City, Abdul Abdallah baada ya kuibuka mabingwa wa kombe hilo kwa penalti 4-3 katika mechi ya fainali dhidi ya Mikocheni United iliyofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Ushindi, Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa timu ya Mikocheni United Keneth Mutta (kulia) akichuana na Jerry Santo wa Mikocheni City katika mechi ya fainali ya kombe la Diwani iliyofanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi Ushindi, Mikocheni, Dar es Salaam juzi. City waliibuka mabingwa kwa mikwaju ya penati 4-3.

MAZOEZI YA KUAGA MWAKA 2012 NA KUKARIBISHA 2013

  Vijana wa jijini Dar es Salaam kutoka klabu za Jogging mbalimbali wakiwa kwenye mazoezi yaliyoanzia kwenye viwanja vya Tanganyika Pekaz Kawe jana, ambapo mazoezi hayo yaliambatana na bonanza kubwa la kuaga mwaka. Bonanza hilo liliandaliwa na Kawe Jogging.


Mbunge wa Kinondoni Iddi Azzan akiwapa mazoezi vijana wa vikundi mbalimbali vya Jogging wakati wa Bonanza la kuaga mwaka lililoandaliwa na Klabu ya Jogging ya Kawe jijini Dar es salaam

 Mbunge wa Kinondoni Idd Azan akishiriki kwenye mazoezi hayo ambayo yalianzia Kawe kuzunguka hadi mbezi kupitia Lugalo na kurejea tena Kawe kwa kupitia Old Bagamoyo road.

RAIS KIKWETE AMJULIA HALI PADRI AMBROS MKENDA ALIYEPIGWA RISASI ZANZIBAR

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar anayeuguza majeraha katika taasisi ya mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) jijijini Dar es salaam leo Jumamosi Dsemba 29, 2012 kukupigwa risasi sehemu za mdomoni na watu wasiojulikana mapema wiki hii  wakati akisubiri kufunguliwa geti  la nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha akiwa pekee yake. Rais Kikwete amempa Padri Mkenda pole nyingi na kumuombea apate nafuu haraka. PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali  Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar anayeuguza majeraha katika taasisi ya mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) jijijini Dar es salaam leo Jumamosi Dsemba 29, 2012 kufuatia kupigwa risasi sehemu za mdomoni na watu wasiojulikana mapema wiki hii  wakati akisubiri kufunguliwa geti  la nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha akiwa pekee yake. Rais Kikwete amempa Padri Mkenda pole nyingi na kumuombea apate nafuu haraka.

TBL YAFANIKISHA UPANDAJI MITI 2600 MWANZA

 Mgeni rasmi katika kampeni ya Mradi wa Upandaji Miti jijini Mwanza, Henry Mongi, akipanda mti  wakati wa kampeni hiyo katika moja ya mitaa ya jiji hilo.Anayeshudia kulia ni Afisa Ubora wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Caroline Muhonoli na wa pili kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mkuyuni, Fasheni Lugo. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia Tanzania. (PICHA NA MDAU BALTAZAR MASHAKA)

 Mgeni rasmi katika kampeni ya Mradi wa Upandaji Miti jijini Mwanza, Henry Mongi, akipanda mti  wakati wa kampeni hiyo katika moja ya mitaa ya jiji hilo.Anayeshudia kulia ni Afisa Ubora wa TBL, Caroline Muhonoli na wa pili kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mkuyuni, Fasheni Lugo.

 Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Steven Kilindo, akifukia udongo kwenye shimo alilopanda mti wakati wa kampeni ya upandaji miti jijini Mwanza mwishoni mwa wiki..Wanaoshuhudia katikati ni Meneja Ubora wa kampuni hiyo, Caroline Muhonoli na nyuma ya Kilindo ni Diwani wa Kata ya Mkuyunim, Lugo Fashen.TBL imetumia zaidi ya milioni 30 kupanda miti 7000 katika mikoa ya Mwanza,Kilimanjaro na Mbeya. Kwa Mkoa wa Mwanza pekee imetumia sh. mil. 10 kupanda miti 2600.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu