Tuesday, May 22, 2018

0 comments

SERIKALI YAWATAKA WADAU WA NGOs KUENDELEA KUTEKELEZA SERA ZILIZO CHINI YA IDARA KUU MAENDELEO YA JAMII

Na Mwandishi wetu Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeawataka wadau wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kuendelea kutekeleza Sera mbalimbali zilizo chini ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii katika utekelezaji wa majukumu yao.
Hayo yamesemwa Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye pia ni Mkurugenzi na Msajili wa NGOs Bw. Marcel Katemba Jijini Dodoma wakati wa  Kikao kati ya Serikali na Wadau hao kinachokaa kwa siku moja kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi zao na kutekeleza Sera zilizo chini Idara kuu Maendeleo Jamii.
Ameongeza kuwa katika kutekeleza Sera mbalimbali Serikali inashirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo nchini ili kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.
Amesema kuwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanafanya kazi kubwa nchini katika kuleta maendelo ya jamii na Taifa katika sekta mbalimbali nchini.
“Wadau wa NGOs mnafanya kazi nzuri na kubwa katika kuleta matokeo chanya kwa jamii na taifa letu” alisisitiza Bw.Katemba.
Kwa upande wake Mwakilishi Kutoka Shirika la World Vision Tanzania Bi. Janeth Edson akitoa mrejesho wa makubaliano kati ya Serikali na NGOs kwa upande wa NGOs amesema kuwa wao kama wadau wataendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza Sera mbalimbali na kuwaasa wadau kuendelea kuunganisha nguvu na Serikali katika kusogeza mbele gurudumu la maendeleo.
MWISHO.
 Mkurugenzi na Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katemba akizungumza na wadau  Mashirika yasiyo ya Kiserikali  yanayotekeleza Sera zilizo chini ya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bi Tausi Mwilima (kulia) akieleza yatokanayo na kikao kilichopita kati ya Serikali na wadau wa NGOs wanaotekeleza Sera mbalimbali zilizo chini ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii  Jijini Dodoma

Mwakilishi kutoka Shirika la World Vision Tanzania Bi Janeth Edson akitoa taarifa kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa hati ya makubaliano ya utekelezaji wa Sera mbalimbali baina ya Serikali na NGOs kwa upande wa NGOs katika kikao kati ya Serikali na wadau hao Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bw. Julius Mbilinyi akitoa mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa hati ya makubaliano na ushirikiano kati ya wadau wa NGOs baina ya Serikali na NGOs kwa upande wa Serikali katika kikao kati ya Serikali na wadau hao Jijini Dodoma.


Endelea Kusoma >>

Sunday, May 20, 2018

MSANII DIAMOND AZINDUA WIMBO WA COLOURS KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI

0 comments
Cathbert Kajuna To:amichuzi,othmanmichuzi,MUHIDIN MICHUZI,Geofrey Adroph Bcc:fungoomar@yahoo.com May 15 at 6:00 AM
Msanii Diamond akipagawisha mashabiki wa Soka waliohudhuria katika Uzinduzi wa wimbo wa Colours maalum kwa ajili ya kombe la dunia 2018 linalofanyika nchini Urusi.
Mkurugenzi wa Coca-Cola Kwanza, Basil Gadzios akiongea machache kuhusu hafla hiyo,(kushoto) ni Meneja wa Coca-Cola nchini, David Karamagi.
Mkurugenzi wa Coca-Cola Kwanza, Basil Gadzios akikata keki wakati wa hafla hiyo. Msanii Diamond akisalimiana na Mameneja Waandamizi wa Coca-Cola. Msanii Peter Msechu na bendi yake wakipagawisha mashabiki wa soka waliohudhuria katika uzinduzi wa wimbo maalum alioshirikishwa msanii Diamond utakaosheresha Kombe la Dunia 2018.
Na Mwandishi Wetu.
MSANII wa Bongo fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewapagawisha vilivyo mashabiki wake wakati akiimba wimbo maalum utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 wimbo uitwao Colours nyimbo aliyoshirikiana na Jason Derulo, katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola Tanzania ni moja ya mdhamini wa mashindano hayo makubwa ya soka duniani na inayofuraha kwa msanii kutoka Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano hayo na kwamba anaimani watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano.
Endelea Kusoma >>

Balozi Dkt. Abdallah Saleh Possi awasilisha hati za utambulisho kwa Baba Mtakatifu Papa Francis, Vatican

0 comments
Balozi Dkt. Possi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin.
 Balozi Dkt. Possi katika picha ya pamoja na Baba Mtakatifu Papa Francis. Wengine ni Afisa wa Ubalozi Bw. Abdul Mhinte, na Mama Balozi, Bi. Sada Mshana.

Balozi Dkt. Possi na Mama Balozi, Bi. Sada Mshana, katika picha ya pamoja na Baba Mtakatifu PaPa Francis
Balozi Dkt. Possi akikabidhi hati za utambulisho kama Balozi wa Tanzania Vatican kwa Baba Mtakatifu Papa Francis.

Balozi wa Tanzania Dkt. Abdallah Saleh Possi, amewasilisha hati za utambulisho kwa Baba Mtakatifu Papa Francis, Vatican tarehe 17 Mei 2018. Pamoja na Ujerumani, Ubalozi wa Tanzania uliopo Berlin pia unahudumia maeneo mengine tisa ya uwakilishi, ikiwemo Vatican.
Kabla ya kuwasilisha hati za utambulisho, Balozi Dkt. Possi alipata fursa ya kukutana na viongozi muhimu wa Vatikani, wakiwemo Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu Mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje na ushirikiano wa kimataifa, Askofu Mkuu Angelo Becciu, Katibu Mkuu Msaidizi wa Vatican.
Mabalozi wengine waliowasilisha hati zao ni pamoja na Balozi Ahmad Naseem Warraich kutoka Pakistan, Balozi Risto Piipponen kutoka Finland, Balozi Lundeg Purevsuren kutoka Mongolia, Balozi RetÅ¡elisitsoe Calvin Masenyetse kutoka Lesotho, Balozi Karsten Vagn Nielsen kutoka Denmark,  na Balozi Sulaiman Mohammed kutoka Ethiopia. 
Baada ya uwasilishaji hati, pia Balozi Dkt. Possi alipata fursa ya kukutana na jumuia ya Watanzania wa Vatican. Dkt. Possi aliwaeleza Watanzania hao kwamba wana jukumu kubwa la kutumia.nafasi zao kuhakikisha nchi ya Tanzania inadumu katika misingi ya uadilifu, umoja, na amani ambavyo ni misingi muhimu ya maendeleo.



Endelea Kusoma >>

CRDB BANK WALIVYOSHIRIKI NA KUTOA HUDUMA KWENYE MAONESHO YA WAJASIRIAMALI WA ILALA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

0 comments
Meneja Biashara wa CRDB Bank, Tawi la Vijana, Zaituni Manora, akitoa sera za benki hiyo kwa wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, wakati wa ufunguzi wa maonesho yao, yaliyofunguliwa na Mkuu wa Wilaya Ilala, Sophia Mjema, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiwa katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.  
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiliandaa gari la kutolea huduma za kibenki katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. 
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo akimwelekeza mmoja wa wananchi aliyefika kwenye banda la benki hiyo katika maonesho hayo, jinsi ya kujaza fomu za miamala ya kifedha ya benki hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya banda lao katika maonesho hayo, wakiwa tayari kutoa huduma kwa wajasiriamali pamoja na wananchi kwenye maonesho hayo, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.   
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo akiwapatia maelezo baadhi ya wananchi waliofika kwenye banda la benki hiyo katika maonesho hayo, jijini Dar es Salaam leo.
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo (kulia), akimpatia maelezo mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Ilala, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kushoto), wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya huduma za kifedha pamoja na ya wajasiriamali kabla ya kuyafungua. 
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kushoto), akimwuliza jambo Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo (kulia), akiwa kwenye banda la benki hiyo, wakati akitembelea mabanda mbalimbali ya huduma za kifedha pamoja na ya wajasiriamali kabla ya kuyafungua maonesho hayo.  
Ofisa Huduma kwa wateja wa CRDB Bank, Makao Makuu, Richard Tangazo (kushoto), akimpatia maelezo mmoja wa wajasiriamali aliofika kwenye banda la benki hiyo, katika maonesho hayo.
Mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, akiwa meza kuu pamoja na baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Ilala kabla ya kuyafungua maonesho hayo.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omar Kumbilamoto, akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema kuzungumza katika ufunguzi wa maonesho hayo. 
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, akizungumza na wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, wakati akiyafungua maonesho yao, viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii, Diwani wa Gongolamboto, Jakob Kisi, akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wa CRDB Bank, Meneja Biashara, Tawi la Vijana, Zaituni Manora, wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo. CRDB Bank, ni moja ya waliodhamini na kufanikisha maonesho hayo ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala.
Endelea Kusoma >>

MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI

0 comments
 NA

PICHA NA OFISI YA BUNGE
Endelea Kusoma >>

Monday, May 14, 2018

0 comments

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Tanzania Emblem RGBWIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO




TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA FAMILIA DUNIANI MEI 15, 2018

Maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani ambayo ufanyika kila ifikapo tarehe 15 Mwezi Mei ya kila mwaka, yataadhimishwa katika ngazi ya Mkoa hapa Nchini huku familia za kitanzania bado zikikabiliwa na changamoto ya mila na desturi zenye madhara na ukatili wa kijinsia na watoto ndani ya familia.

Taarifa ya vichocheo vya ukatili nchini  ya mwaka 2015 inaonesha kwamba wanaotekeleza vitendo vya ukatili ni watu wa karibu na familia au wanafamilia wenyewe. Aidha, taarifa ya vitendo vya ukatili vilivyoripotiwa na Jeshi la polisi kwa mwaka 2017 vilikuwa 13,457.

Ili kukabiliana na madhara na changamoto zitokanazo na vitendo hivi vya ukatili katika ngazi ya familia na jamii kwa ujumla Serikali imeandaa kitini cha malezi kwa ajili ya  kutoa elimu malezi na hatimaye kupunguza matukio ya ukatili katika ngazi ya familia.

Juhudi ya kutoa elimu ya malezi katika familia itasaidia wazazi kuwa na mbinu za kuweka mazingira rafiki kwa watoto na ikiwa ni pamoja na kutenga muda wa kutosha kukaa na kujadiliana masuala mbalimbali kwa lengo la kujenga mahusiano yatakayowandaa kudumisha fikra za uzalendo, utu na maadili mema katika kutumia familia zao na Taifa kwa ujumla.  

Hadi sasa mafunzo hayo yametolewa kwa wazazi 3,600, viongozi wa Serikali za vijiji 113, Maafisa Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii Kutoka Halmashauri 76, wanafunzi 10,046, walimu 486, viongozi wa dini 110, wazee wa mila 90, ngariba 38 na  waendesha bodaboda 361.
Uelewa mdogo wa wanafamilia na jamii kuhusu malezi yanayofaa kwa watoto na mbinu za kuimarisha mahusiano miongoni mwa wanafamilia huathiri ukuaji wa watoto na kupelekea watoto kukosa mahitaji muhimu katika familia na hatimaye kukimbia nyumbani. Kupitia kitini cha elimu ya malezi, familia zitaweza kuboresha malezi na familia kuendelea kuwa mahali salama panapofaa kuishi.

Kupitia Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto 2017/18 – 2021/22, Wizara imeunda vikundi vya malezi na kutoa elimu ya malezi katika familia 800 za mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya. Wizara itaendelea kuhamasisha uundaji wa vikundi katika mikoa mingine ili kuimarisha wajibu wa malezi katika familia.

Jamii imekuwa na mtazamo hasi kuhusu malezi  na hivyo kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili kwa watoto na vijana. Utamaduni wa familia tandaa kushirikiana katika malezi umekuwa ni changamoto kwa wakati huu kutokana na kukosa mwitikio wa uwajibikaji katika malezi ya wanafamilia katika jamii.

Matokeo yake baadhi ya watoto wa mekuwa wanajilea wenyewe pale wanapofiwa na wazazi, wazee nao wanakosa matunzo stahiki na wenye ulemavu wamekuwa wakitaarifiwa kufungiwa ndani. Wakati tunaadhimisha Siku ya Familia Duniani kwa mwaka 2018, wazazi na walezi wanatakiwa kuzingatia upendo na mahusiano mema ndani ya familia ili kujenga familia na jamii iliyo bora na yenye maadili.

Siku hii huadhimishwa na Nchi Wanachamawa Umoja wa Mataifa kwa mujibu wa Tamko Namba 47/237 la Umoja wa Mataifa la tarehe 20 Septemba, 1993. Kwamatinki hiyo madhumuni ya maadhimisho haya nikutambua umuhimu wa familia kama chanzo cha jamii. Kaulimbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Malezi Jumuishi: Msingi wa Uzalendo, Utu na Maadili ya Familia na Taifa”.

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
(Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii)
13/05/2018

Endelea Kusoma >>

KILIMANJARO BIA YA TANZANIA KINYWAJI RASMI KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI

0 comments
 Meneja wa kiwanda cha Ilala, Calvin Martin na Meneja Masoko George Kavishe, wakiongoza wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa promosheni ya bia ya Kilimanjaro kufanya cheers
 Maofisa waandamizi wa ABinBev wakifuatilia matukio na shamrashamra wakati wa hafla ya uzinduzi
 Wageni waalikwa na wafanyakazi wa TBL wakiburudika wakati wa uzinduzi huo
 Shamrashamra mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi
 Shamrashamra mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi
Wageni mbalimbali wakifuatilia matukio na kupata burudani wakati wa uzinduzi. *Kuwazawadi wateja wake kushuhudia mechi za mashindano hayo Live Kampuni ya Tanzania Breweries Limited mwishoni mwa wiki imetangaza ushirikiano wake na shirika la Soka Duniani (FIFA), ambapo bia yake ya Kilimanjaro, imetangazwa kuwa bia rasmi ya Tanzania katika mashindano ya Kombe la Dunia 2018 yatakayofanyika nchini Urusi. Kutangazwa huku kunaenda sambamba na kuzinduliwa kwa promosheni kubwa ya kwanza na ya aina yake nchini Tanzania itakayowazawadia wateja wa bia ya Kilimanjaro nafasi ya kujindia safari ya kushuhudia baadhi mechi za kombe la dunia nchini Urusi mubashara na pia kujishindia muda wa maongezi 2,500/= kila wanaponunua bia ya Kilimanjaro na kushiriki mara (sita) 6 kutuma number iliyopo chini ya kizibo kwenda 15451 fedha taslimu kiasi cha shilingi 1,000,000/- Kila wiki kwa wiki Kumi. Hafla kubwa ya uzinduzi iliyojumuisha wafanyakazi wa TBL,Waandishi wa habari,wasanii na wadau mbalimali wa kampuni ilifanyika katika kiwanda cha TBL cha Ilala jijini Dar es Salaam ambapo uzinduzi utaendelea kufanyika katika mikoa mingine Meneja Masoko, udhamini na program za wateja Afrika Masharariki wa kampuni ya TBL Group Bwana George Kavishe alisema “Tunayo furaha chapa yetu maarufu ya Kilimanjaro kutangazwa kuwa bia rasmi ya Tanzania katika msimu huu wa kombe la Dunia la FIFA 2018, kampuni inatangaza kuzindua kampeni maalumu ambayo itawawezesha wateja watakaobahatika kushinda kugharamiwa safari ya kwenda Urusi kuangalia mechi za kombe la Dunia mubashara sambamba na zawadi za fedha taslimu kiasi cha shilingi Milioni moja kila wiki, muda wa maongezi 2,500 kila unaposhiriki kutuma number iliyopo chini ya kizibo mara 6, pamoja na zawadi kem kem zitakazotolewa kwenye promosheni za kwenye mabaa zaidi ya mia tatu nchi nzima. Alisema washindi wapatao 10 watawezeshwa kugharamiwa kuona mashindano ya kombe la Dunia na washindi wengi wataweza kujishindia fedha taslimu, na muda wa maongezi. “Lengo kubwa la promosheni hii ni kuwazawadia wateja wetu ili waburudike katika msimu huu wa shamrashamra za kombe la dunia la FIFA 2018”.Alisisitiza Ili kujishindia zawadi mteja anapaswa kutuma namba zilizopo kwenye chupa za bia ya Kilimanjaro kwenda namba 15451 ili kujipatia fedha taslimu na muda wa maongezi, Zawadi ya ticket ni kwa wale wataoshiriki kujibu maswali yatakayoendeshwa kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya www.Kililager.com na kujipatia point za ushindi. Promosheni hii itadumu kwa muda wa miezi miwili na nusu na litaendeshwa nchi nzima na matangazo yake yamezinduliwa rasmi pia kupitia televisheni, radio na mitandao ya kijamii. --
Endelea Kusoma >>

DC GAIRO AAGIZA WACHIMBAJI MADINI WASIO NA LESENI KUSIMAMISHA UCHIMBAJI MARA MOJA

0 comments
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama mara baada ya kutembelea sehemu ya migodi inayochibwa kinyemela na wachimbaji wasiokuwa na leseni.
Moja ya mashine zilizokutwa eneo la mgodi. Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe amesikitishwa na makampuni ya uchimbaji madini ya viwandani wanaochimba madini mbalimbali Wilayani hapo hasa aina ya Felispar bila leseni. Mhe. Mchembe aliyasema hayo alipotembelea migodi ya Kata ya Rubeho ambapo wachimbaji wameweka mashine nzito na wanafanya kazi wakati hawana leseni. Sheria ya Madini ya mwaka 2010, kifungu cha 18 kimeweka bayana adhabu kwa mchimbaji haramu. Ikiwa ni mtu binafsi faini isiyozidi milioni 5 au kifungo miaka mitatu au vyote pamoja. Kama ni kampuni basi ni faini isiyozidi shilingi milioni 50. Mheshimiwa Mchembe aliendelea mbali na kuelezea kifungu cha 6 (4) cha Sheria ya Uwazi na Uwajibikaji namba 29 ambapo madini yaliyopatikana kupitia uchimbaji haramu yatataifishwa na Serikali chini ya Kamishna wa madini na kuuzwa kwa mnada. Mitambo yote pia inapaswa kutaifishwa. Akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya Mhe. Mchembe ametoa maagizo hayo na kumtaka Afisa Madini Mkoa na Kanda kufatilia jambo hilo kwa karibu. Pia amepiga marufuku raia wa kigeni kutembelea maeneo ya machimbo bila kibali. Aidha uzingatiwaji wa kanuni 3 (1) (2) ambapo mchimbaji anatakiwa kuwasilisha kwa Afisa Madini mkazi kanda taarifa ya tathmini na mpango wake wa utunzaji wa mazingira kabla ya kuanza kuchimba madini. Wilaya ya Gairo ina madini aina mbalimbali na maeneo ya milimani yameachwa na mashimo makubwa.
Endelea Kusoma >>

COCA-COLA BONITE YAZIDI KULETA RAHA YA MZUKA WA SOKA NA COKA KANDA YA KASKAZINI

0 comments
 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
Mmoja wa washindi wa fedha taslimu akipokea zawadi yake Wakati mashindano ya kombe la Dunia 2018 yanakaribia, kampuni ya Coca-Cola Bonite Bottlers Limited ya mjini Moshi inazidi kumwaga zawadi za pikipiki,luninga za kisasa na fedha taslimu kwa wakazi wa Kanda ya Kaskazini kupitia promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka inayoendelea. Akiongea katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi 16 wa wiki liyopita, Meneja Mauzo wa Bonite, mkoa wa Arusha Bw. Boniphace Mwasi, alisema zaidi ya wateja 50 wamejishindia zawadi na zawadi bado ziko nyingi. “Bado tunazo zawadi nyingi hivyo natoa wito kwa wakazi wote wa kanda ya kaskazini kuchangamkia kunywa soda za Coca-Cola, ili waweze kujishindia zawadi”. Wakiongea muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi zao washindi waliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa kubuni promosheni zenye mwelekeo wa kuleta furaha kwa jamii hususani kwa kuwakwamua kiuchumi. --
Endelea Kusoma >>

Tuesday, April 24, 2018

VICENT MBILINYI AJINOWA KUMKABILI HUSSEIN SHEMDOE MEI MOSI TANDIKA

0 comments



Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kulia akimnowa bondia vicent Mbilinyi kwa kumuelekeza kupiga ngumi ya mkunjo wa chini 'Upcat' Mbilinyi anajiandaa na mpambano wake na Hussein Shemdoe utakaofanyika katika ukumbi wa musoma Bar siku ya Mei Mosi Picha na SUPER D BOXING NEWS
Na Mwandishi Wetu

BONDIA Vicent Mbilinyi amendelea na mazoezi ya kumkabili Hussein Shemdoe wakati wa mpambano wao utakaofanyika mei mosi siku ya sikukuu ya wafanyaklazi Dunian mpambano uho utafanyika katika ukumbi wa Musoma Bar uliopo Tandika Mwembe Yanga mpambano wa raundi 8

Mbilinyi anaenolewa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amekuwa nje ya ulingo kwa mda wa mwaka mzima sasa tangu mwishoni mwa mwaka 2016 na sasa anakuja kivingine

mbali na mpambano huo siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya mabondia mbali mbali ambapo bondia Shafii Ramadhani atapambana na Antony Mathias wakati Nassibu Ramadhani atavaana na Hamisi Mohamedi na Shomari Galibu atapambana na Hashimu Sheni wakati Said Mlugulu atavaana na Said Bakari 'Kidedea' 

Mapambano haya yoteyatafanyika siku hiyo katika ulingo mpya  wa mdau wa masumbwi nchini Zahoro Maganga 'Super Diego' aliejenga ulingo uho kwa ajili ya kuwakombowa mabondia na hadha ya kupigania chini 

siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua

mpaka kujua kitu kamili katika

mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd


Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani
-- 

Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu