Sunday, January 27, 2013

MBUNGE WA MOROGORO AKITEMBELEA BWAWA LA MINDU

mbunge wa jimbo la morogoro mjini Abdullazizi Abood akitembelea draja
DHI ya wakazi wa Manispaa ya Morogoro,wameupongeza utendaji kazi wa Mbunge wa jimbo lao Abdulaziz Abood,(CCM)kutokana na kufanya ziara za kustukiza katika maeneo yanayolalamikiwa na wananchi.

Miungoni mwa maoneo yaliyolalmikiwa siku za hivi karibuni ni pamoja na maji yanayosambazwa na mamlaka ya maji safi na maji taka yanayotoka katika mabomba kuwa machafu ambapo Mbunge huyo alifanya ziara ya kustukiza katika bwa la mindu na kuagiza uongozi wake kurekebisha hali hiyo kitu ambacho kilifanyika.
Eneo lingine ni pamoja na Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro ambapo wanachi walilalamikia huduma duni na lugha chafu zinazotolewa na wauguzi kwa wagonjwa na Mbunge huyo kulazimika kufika katika eneo hilo na kushuudia hali hiyo baada ya kuelezwa na wagonjwa walilazwa katika  wodi mbalimbali.
Hata hivyo kufuatia hali hiyo ilimlazimu Mbunge huyo  kuzungumza na uongozi wa Hospitali hiyo ili waweze kukemea wauguzi wenye tabia hiyo kwani wagonjwa wanahitaji kupewa faraja.
Wakizungumza na Waandishi habari  mjini hapa ,wanachi hao wanaoishi maeneo ya kihonda walisema katika kipindi cha takribani mwezi mmoja mamlaka ya majisafi na maji taka Moruwasa bila huruma imekuwa ikiwanywesha maji machafu yenye rangi ya kijani,yanayowasha na yanayotoa povu pindi wanapoyachemsha.
“Nampongeza Abood kwa ziara yake maana zaidi ya mwezi mmoja wananchi tulikuwa tunakunywa  maji machafu kupita kiasi hadi kubadilika kuwa na rangi ya kijani na ukiyachemsha yanatoa povu kama maji ya kufulia nguo sasa amejionea uhalali wa malalamiko ya wananchi kuhusu tatizo hili la maji”. alisema Agnes Julius  mkazi wa  kihonda Magorofani.
Naye  Ramadhani Omary  mkazi wa Kichangani alisema kuwa utendaji wake umesaidia kutatua kero katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambako wauguzi wamekuwa wakitoa lugha chafu kwa wagonjwa.
Kwa upande wake Abood alisema kuwa yeye amechaguliwa na wananchi hivyo atahakikisha anatetea na kupigania maslahi ya yao huku akisisitiza kumpa ushirikiano kuweza kufikia malengo hayo.
“ Mimi nimegombea ubunge kwajili ya kutetea maslahi ya wananchi wa Morogoro,hivyo siku zote nitakuwa upande wao “ alisema Abood.
Mwisho

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu