International
Boxing Federation
Africa
IBF/AFRICA
FOR IMMEDIATE RELEASE - Thursday, February 28, 2013 - Dar-Es-Salaam, TANZANIA-
Siku kubwa na yenye matumaini mapya katika maisha ya bondia
wa Namibai Albinus Felesianu (9(4)-2(1)-0)
itawadia hivi karibuni wakati atakapokutana na
bodia Herbert
Quartey (10(7)-8(6)-0) wa Ghana kugombea ubingwa wa IBF wa dunai uzito wa Unyoya
(Featherweight).
Albinus alipata mshtuko mkubwa sana na kushangzwa na habari
za hivi karubunI kuwa IBF imempa nafasi ya kugombea ubingwa wa dunia wa vijana
jambo lililomfanya apate furaha ya ajabu.
Albinus (kushoto) akifanya vitu vyake
Mtu pekee atakayeweza kuzima furaha yake na kumfanya asiweze
kufikia malengo yake katika ngumi ni bondia Herbert Quartey kutoka Ghana ambaye
ni moja kati ya mabondia wenye ujuzi mubwa wa kupigana ulingonI.
Kama inavyosemwa kuwa "mtoto mtukutu aliyepotea kwenye ngumi anapoomba
kurudi kundini na kukaa kufuata kanuni na shaeia za ngumi mchezo wa ngumi humpokea
kwa shangwe na nderemo na kumpa mawaidha na ushauri wa kumwendeleza" ndivyo
hivyo hivyo Albinus Felesianu na Herbert Quartey watakavyopokelewa na ngumi
baada ya pambano lao la tarehe 29 Machi jijini Windhoek, Namibia.
Bondia Albinus Felesianu yuko chini ya promosheni ya Kinda Nangolo ambaye anamiliki kampuni
tanzu ya Kinda Boxing Promotion na ni promota anayeinukia kwa kasi sana katika
tasnia ya ngumi nchini Namibia na barani Afrika.
ISSUED BY:
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
Benjamin William Mkapa Pension Towers
Tower B, Mezzanine Floor, Azikiwe Street
Dar-Es-Salaam - Tanzania
Dar-Es-Salaam - Tanzania
0 comments:
Post a Comment