Thursday, February 28, 2013

WATEJA WA NMB SASA KUWEKA FEDHA KUPITIA M- PESA

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa NMB Mark Wiessing,( kulia) na  Ofisa Mkuu wa Biashara- M-Pesa- Jacques Voogt wakitiliana saini mkataba wa ushirikiano na makubaliano ya kuwawezesha wateja wa benki ya NMB kufanya muamala wowote kwenye akaunti zao kwa kutumia huduma ya M-Pesa. Kulia ni Imman Kajula kutoka Benki ya NMB na (kushoto) ni Kelvin Twisa  wa Vodacom, na maofisa wengine wawili (katikati) pia wakishuhudia.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa NMB Mark Wiessing, (kulia) na  Ofisa Mkuu wa Biashara- M-Pesa- Jacques Voogt wakibadilishana mkataba baada ya kutiliana saini kama ishara ya ushirikiano na makubaliano ya kuwawezesha wateja wa NMB kufanya muamala wowote kwenye akaunti zao kwa kutumia huduma ya M-Pesa. Hafla hiyo ya kutiliana saini kataba huo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
*************************************************************
BENKI ya NMB leo imeweka historia  kwa kuanzisha huduma mpya itakayowawezesha wateja  wake nchini kote kuweza kuweka amana zao kupitia mawakala zaidi ya 40,000 wa huduma ya M-Pesa. Pia wateja wa NMB wataweza kutuma fedha kutoka NMB kwenda MPESA.  NMB na Vodacom zimeshirikiana katika huduma hiyo na kuzindua rasmi huduma hiyo katika hafla fupi iliyofanyika leo mchana katika Ofisi za Makao Makuu ya Benki hiyo ya NMB, jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuzinduliwa kwa huduma hiyo Sasa mtu yeyote ama wateja wa NMB hawatahitaji kwenda ndani ya benki ili kuweka fedha kwenye akaunti kwani sasa wataweza kuweka fedha katika akaunti ya NMB bila kwenda tawini.  Pia sasa wateja zaidi ya 800,000 wa NMB mobile wataweza kutuma fedha kwenda MPESA.



Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo, jijini Dar es Salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Mark Wiessing, “alisema “Ni huduma ya aina yake ambayo itawezesha mzunguko wa miamala baina ya wateja na benki ya NMB kufanyika kwa urahisi na haraka, jambo litakalosaidia kwa kiasi kikubwa kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki sanjari na kuboresha hali ya maisha na uchumi kwa watanzania wote mijini na vijijini”.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu