Sunday, April 28, 2013

MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

 Marais wa jumuiya ya Afrika Mashariki wakisimama kwa dakika moja kumkumbuka laiyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Uganda Marehemu Eriya Kategaya wakati wa ufunguzi wa kikao cha kumi na moja cha Jumuiya hiyo jijini Arusha leo mchan. Katika Hoteli ya Ngurdoto.Kutoka kushoto Rais Wa Burundu Pierre Nkurunzinza,Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya wakati wa ufunguzi wa kikao cha juu cha kumi na moja cha Wakuu wa nchi wa jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofaniyka jijini Arusha.
 Marais  Wa jumuiya ya Afrika Mashariki waliohudhuria Mkutano wa Wakuu wa jumuiya hiyo katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha leo.Kutoka kushoto ni Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi,Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda,Mwenyeji wa mkutano Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mpya wa Kenya,Uhuru Kenyatta(picha na Freddy Maro)
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Mkewe Margareth Kenyatta wakifurahia ngoma za utamaduni muda mfupi bbada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijijini Arusha(picha na Freddy Maro)

Rais .Jakaya Kikwete akimkaribisha Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowasili juzi jioni kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuia ya Afrika ya Mashariki unaofanyika jijini Arusha. (PICHA NA FREDDY MARO)
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu