Thursday, September 26, 2013

KARAMA NYILAWILA KUZIPIGA OCTOBA 20


Karama Nyilawila
BONDIAw a ngumi za kulipwa nchini, Karama Nyilawila aliyewahi kuwa bingwa wa dunia wa WBF uzito wa middle anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi ujao kuzipiga na Sado Philemon.
Nyilawila aliyempiga Kreshnik Qato wa Czech wakati akitwaa taji lake la WBF ambalo alilitema baada ya kushindwa kwenda kulitetea ili apate nafasi ya kuzipiga kirafiki na Francis Cheka mjini Morogoro na kudundwa, atazipiga na Philemon kwenye ukumbi wa CCM Mwinjuma siku ya Oktoba 20, pambano lililoandaliwa na kampuni ya Bigright Promotion.
Mratibu wa pambano hilo, Ibrahim kamwe alisema kuwa maandalizi mpaka sasa yanaenda vizuri.
Hata hivyo Kamwe alisema mabondia wanaendelea kujifua kimkandamkanda kutokana na kukosekana kwa wadhamini na hasa mabondia watakaosindikiza pambano hilo.
Kamwe alisema Nyilawila na mwenzake wameshasaini makubaliano ya kupanda ulingoni siku hiyo ambapo watasindikizwa na michezo kadhaa itakayohusisha mabondia chipukizi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu