Sehemu
ya mamia ya wananchi wa Kata ya Mjini, Manispaa ya Songea wakiwa tayari kwa
kumsikiliza Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi. Dk Nchimbi baada ya kuzindua barabara
yenye kiwango cha lami yenye urefu wa mita 600 ambayo imegharimu zaidi ya Sh75
milioni, pia mbunge huyo ameweka jiwe la msingi katika ofisi ya Kata ya Mateka.
Dk Nchimbi katika ziara yake ya siku tano jimboni humo, pia anatarajiwa
kuzindua ujenzi wa mabweni ya sekondari pamoja na nyumba za walimu.
|
0 comments:
Post a Comment