Monday, February 24, 2014

ZUNGU LA UNGA LAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA LEO


Raia wa Henellic, Alexamdrios Atanasios, amekamatwa  maafisa wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Jumapili usiku Februari 24, 2014, akiwa na kilo tano za madawa ya kulevya.

Kwa mujibu wa duru za kiusalama uwanjani hapo, raia huyo alikamatwa wakati wa upekuzi, akijiandaa kupanda ndege ya Swiss air akielekea mjini Zurich.

Kwa mujibu w aduru hizo za usalama, madawa hayo yalikutwa yakiwa yamefichwa kwenye “sakafu” ya begi lake baada ya mitambo ya kisasasa ya upekuzi, kugundua kuwa kulikuwa na ‘mzigo’.

Habari zinasema, kwa sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwenye kituo cha polisi cha uwanja wa ndege akisubiri taratibu za kisheria ili afungukliwe mashtaka.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu