BRAZIL `WACHIZIKA` NA USHINDI WA PENATI DHIDI YA CHILE, SASA NGOMA ROBO FAINALI!
wakishangilia ushindi wao wa
penati 3-2 dhidi ya Chile na kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali.
WENYEJI Brazil wamekuwa wa kwanza kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe
la dunia baada ya jana usiku kuifunga Chile kwa mikwaju 3-2 ya penati
kufuatia sare ya bao 1-1 katika dakika 90 za kawaida na dakika 30 za
nyongeza.
Kutokana na matokeo hayo, baadhi ya wachambuzi wa soka wameanza kuwa na
wasiwasi na mwendo wa Brazil na kushindwa kutambua watafika hatua gani.
Lakini sapoti kubwa wanayopata kutoka kwa mashabiki wao inaweza kuwa
motisha kubwa kwao na wakajikaza hatua inayofuata.
Jibu...
0 comments:
Post a Comment