Wednesday, December 31, 2014

KOCHA MPYA SIMBA ATUA DAR, AKATAA KUIZUNGUMZIA YANGA



Kocha mpya wa Simba, Goran Kopunovic ametua jijini Dar es Salaam, tayari kuanza mazungumzo na uongozi wa Simba.

Lakini Kuponovic amekataa katakata kuizungumzia Yanga na kusema akili yake ni Msimbazi.

"Siwezi kuizungumzia Yanga, najua mambo ya upinzani yapo lakini kwa sasa naelekeza nguvu zangu katika mechi ya kwanza.

"Kama nitasaini na Simba, basi nitaangalia nitafanya nini katika mechi ya kwanza," alisema Kopunovic raia wa Serbia mara tu baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu