Charles Mihayo akishikiliwa na polisi |
MTANZANIA
anayeishi nchini Austaralia, Charles Mihayo ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi
ya kuwaua kikatili watoto wake mwenyewe ili kumkomoa mkewe aliyekuwa ameachana
naye amehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mihayo
mwenye miaka 36, alifanya ukatili huo kwa wanae Savannah (4) na Indianna (3)
Aprili 20, 2014 nyumbani kwake huko Melbourne na amehukumiwa leo kifungo hicho.
Inadaiwa
kuwa baada ya kuachwa na mke wake, hasira zilimfanya bwana Mihayo kuamua
kufanya ukatili wa kukatisha uhai wa watoto wake mwenyewe Savannah (4) na
Indianna (3), ili tu kumuumiza mke wake kama njia ya kumlipizia kisasi.
Inadaiwa kuwa aliwauwa kwa kuwakandamiza na mto baada ya kucheza nao.
Taarifa
hiyo inaeleza kuwa siku mauaji hayo yalipofanyika, mama wa watoto hao
aliwapeleka kwa baba yao bwana Mihayo. Baada ya kuwafikisha baba yao
aliwafanyia shopping ya nguo na viatu vipya.
Kabla ya
kutenda ukatili huo kwa damu yake mwenyewe, Mihayo aliwarekodi video wakicheza
muziki huku akicheza nao. Na katika video ambayo polisi baadae waliiona,
alisikika akiwaambia binti zake wamuoneshe mama yao nguo mpya alizowanunulia,
na walifanya hivyo na kisha mwanaume huyo akakaa mbele ya camera na kusema
“tutamuonesha mama kitu kingine dakika kumi zijazo”, na kuendelea kucheza nao
hadi alipowakandamiza na mto (pillow) hadi kufa.
Baada ya
kufanya mauaji Mihayo mwenyewe aliwapigia simu polisi ambao baada ya kufika
nyumbani kwake wakiwa mlangoni aliwaambia , “Tayari, nimewaua. Nimewaua watoto
wangu. Inabidi mumuulize huyu [mama yao] sababu.”
Polisi
waliwakuta watoto hao wakiwa tayari wamefariki huku wakiwa wamevalishwa nguo na
viatu vipya ambavyo walinunuliwa na baba yao siku hiyo.
Licha ya
kuhukumiwa kifungo cha maisha, Charles Mihayo anatakiwa kutumikia kifungo cha
miaka 31 kabla ya kupata haki ya kupewa msamaha.Savannah (4) kulia na Indianna (3) kushoto |
Savannah (4)kulia na Indianna (3) |
0 comments:
Post a Comment