WAZIRI Mkuu wa zamani Mh. Edward
Lowassa, (kulia), akionyesha mkoba wenye fomu za kuomba kuwania urais
kupitia CHADEMA, baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mh.
Freeman Mbowe, kwenye makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar
es Salaam, leo Julai 30, 2015. Mh Lowassa, alijiunga hivi karibuni na
chama hicho, baada ya kujitoa CCM
Mh. Lowassa, akipokea mkoba wenye fomu
hizo kutoka kwa Mwenyekiti Mbowe, huku Mama Regina Lowassa, mke wa Mh.
Lowassa, akishuhudia
Mh. Lowassa, akiteta jambo na
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu, na Naibu Katibu Mkuu wa chama
hicho, (Zanzibar), Salum Mwalimu
Baadhi ya wafuasi wa CHADEMA, wakionyesha kadi za kupigia kura kwenye
uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2015, wakati wakisubiri kumuona Mh. Lowassa,
makao makuu ya CHADEMA jijini Dar es Salaam Julai 30, 2015
Mh. Lowassa, akiongozana na Mkewe, wakati akiwasili makao makuu ya CHADEMA, Kinondoni jijini Dar es Salaam Julai 30, 2015
Mh. Lowassa, akiwapungia mkono wafuasio
wa CHADEMA, wakati akiondoka makao makuu ya chama hicho, baada ya
kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa na chama hicho kuwania urais wa
Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015
Mh. Lowassa, akitoa hotuba baada ya kuchukua fomu
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, akihutubia kwenye hafla hiyo
Mh. Lowassa, "akipiga" People's..................Power
WAZIRI MKUU MSTAFF EDWARD LOWASSA KATIKA SAFARI MATGEGEMEO AKILAKIWA CHADEMA LEO |
0 comments:
Post a Comment