Sunday, October 4, 2015

MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA AFARIKI DUNIA

ISOME HAPA SAFARI NZIMA YA MAISHA YA MAREHEMU MCH.MTIKILA


Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila amefariki dunia leo alfajiri kwa ajali ya gari katika Kijiji cha Msolwa,


Imeandaliwa na Mzee wa matukio daima.


MCHUNGAJI Christopher Mtikila ni Mwenyekiti wa chama cha Democratic Party (DP) ambacho kina usajili wa kudumu hapa nchini. 


Mtikila alizaliwa mwaka 1950 mkoani Iringa, kusini mwa nchi yetu.

(Kwa bahati mbaya, hadi nachapisha uchambuzi huu sikupata taarifa za elimu yake) kwani hakuwa mwepesi kutoa ushirikiano mwezi mmoja uliopita alisafiri kwenda nje ya nchi na kurejea wakati nikiwa katika hatua za mwisho za uhariri.


Pamoja na shughuli za siasa, Mchungaji Mtikila ni mwanzilishi na mkuu wa kanisa la Kipentekoste la Full Salvation Church. Lakini pia kwa muda mkubwa wa maisha yake amekuwa anajihusisha sana na harakati za haki za binadamu kwa kupitia kitengo cha haki za binadamu cha kanisa hilo kiitwacho “Liberty Desk”. 
Kanisa lake ni moja ya makanisa machache sana hapa Tanzania yenye vitengo vya namna hiyo.
Umaarufu wa Mtikila ulikua sana mwanzono mwa miaka ya 1990 kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuongea, upinzani wake dhidi ya muundo wa muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, madai yake kuhusu kile anachokiita “uhujumu wa uchumi unaofanywa na wahindi” (ambao anawaita Magabacholi), na kesi mbalimbali za kikatiba alizokuwa akifungua katika mahakama za Tanzania,ni kati ya mambo machache yaliyofanya asikike kila kona ya nchi.
Kwa muda mrefu chama chake cha DP hakikuweza kupata usajili wa kudumu kutokana na kukataa kwake kuitambua Zanzibar, alikuwa akisisitiza kuwa chama chake ni cha Tanganyika na sio Tanzania. 

Hata hivyo Mtikila ilimpasa abadili msimamo wake katika miaka ya hivi karibuni kwa kukubali kutafuta wanachama toka Zanzibar (kama sheria ya uchaguzi inavyotaka) na hivyo chama chake kilipata usajili wa kudumu.


Mtikila alifungwa kwa mwaka mmoja mwaka 1999 baada ya kupatikana na hatia ya kutoa maneno ya kashfa dhidi ya aliyekuwa katibu mkuu wa CCM, marehemu Horace Kolimba. 

Mwaka 2004 pia alihukumiwa kifungo kilichosimamishwa cha miezi sita kwa kutoa maneno ya kashfa dhidi ya mkuu wa polisi wa wilaya ya Ilala. Kwa ujumla maisha yake yamekuwa ni ya harakati muda wote, akipambana awezavyo, akisimama kidete inavyowekana na akijikuta matatani kila uchwao. Mchungaji Mtikila amemuoa Bi. Georgia na wana watoto.

MBIO ZA UBUNGE

Mwaka 1997, Mbunge wa jimbo la Ludewa kwa tiketi ya CCM, Horace Kolimba aliitwa na Kamati Kuu ya chama chake mjini Dodoma kwenda kujibu mashtaka ya ndani ya chama juu ya kauli ambazo alikuwa akizitoa kwamba “CCM imepoteza mwelekeo”, baadhi ya viongozi wa chama chake walimchukulia kama msaliti na wengine wakimuona kama mtu aliyethubutu kusema ukweli bila kumuhofia Nyerere.


 Kusoma zaidi bofya HAPA.
Share this article :

1 comments:

  1. http://ituhambeya.blogspot.com/2015/10/angalia-video-kauli-za-mch-christopher.html

    ReplyDelete

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu