Saturday, March 12, 2016

PINGAMIZI LA MBUNGE WA TEMEKE ABDALLAH MTOLEA



 Katibu mwenezi Kata ya Miburani  Ally Kamtande, akizungumza na wafuasi wa Kamanda wa wa Vijana Mkoa wa Dar es Salaam jana baada ya Kesi ya msingi iliyofunguliwa na Mbuge wa Jimbo la Temeke  Abdallah Mtolela, akiiomba mahakama ifutilie mbali shauri lililofunguliwa na Kamanda wa Vijana Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu, (PICHA ZOTE NA UJIJIRAHAA BLOG)

 Kamanda wa Vijana Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu akitoka Mahakamani  mara baada ya kesi kuahirishwa hadi Machi 24, 2016
Kamanda wa Vijana Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu akiwa na wanachama wake waliojitokeza kumsindikiza Mahakamani.


KESI ya pingamizi iliyofunguliwa na Mbunge wa Temeke Abdallah Mtolea dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Abbas Mtemvu imeahirishwa hadi Machi 24 mwaka huu.Hayo yalisemwa na Katibu Mwenezi wa kata ya Miburani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Temeke, Ally Kamtande wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho ambao walijitokeza katika Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.Kamtande, aliwataka wanachama wa CCM kumuomba Mungu ili ikifika Machi 24 kesi hiyo isikilizwe na kuwapatia hukumu nzuri.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu