KANU AONDOKA NCHINI NA KUACHA MENGI YA KUJIFUNZA
Na Dotto Mwaibale
Baada ya kufanya ziara
katika sehemu mbali mbali nchini toka alivyoingia tarehe 6 Aprili akitokea
nchini Kenya, balozi wa Afrika wa StarTimes, Nwankwo Kanu aondoka nchini huku
nyuma akiacha somo kwa wanasoka wote wa Tanzania.
Katika ziara alizofanya,
Kanu kila alipopita aliwapa vijana morari ya kuweza kupambana hasa katika
michezo hususani mpira wa miguu ili nao waweze kufanikiwa kupitia michezo.
Kanu aliwahamasisha
vijana haswa wanaopenda mpira wa miguu kujitoa na kuupenda mchezo huo kutoka
moyoni. “Mimi nimeanza kucheza mpira nikiwa sina viatu lakini niliufurahia
sababu niliupenda toka moyoni”, alisema Nwankwo Kanu.
Alibainisha kuwa ili
kuwa mchezaji bora wa mpira wa miguu ni lazima mchezaji uwe na vitu muhimu vya
kufuata kama vile nidhamu, juhudi na heshima mchezoni.
“Nilikuwa na nidhamu,
niliupenda mpira, juhudi za mazoezi na heshima pia ndiyo maana nilifanikiwa na
kuchezea vilabu vikubwa duniani ikiwemo Inter Milan na Arsenal. Sasa hivi
wazazi wangu wanaishi maisha mazuri.” Nwankwo Kanu, aliwapa morari vijana
waliokuwa katika kituo cha michezo cha Jakaya Mrisho Kikwete kilichopo jijini
Dar es Salaam.
Balozi huyo wa StarTimes
katika ziara alizozifanya ndani ya siku tano nchini, alitembelea hospitali ya
Muhimbili na kupita katika Wodi ya wagonjwa wa moyo na kuahidi kutoa
ushirikiano mkubwa na hospitali hiyo ili kuweza kuisaidia kadri awezavyo
akihihusisha pia StarTimes kuangalia jinsi gani inaweza rusha matangazo ya
kuelimisha kuhusiana na magonjwa mbali mbali ya moyo. Ukizangatia na yeye ana
matatizo hayo ambayo yalimpelekea kuanzisha taasisi yake ya moyo, The Kanu
Heart Foundation, ambayo inawasaidia watu wengi huko kwao Naijeria hivi sasa.
“Tutaangalia kwa ukaribu
zaidi ni jinsi gani tutasaidiana ila mimi pia nikiwa kama balozi wa StarTimes
nitafanya jitihada za lazima kuona nitasaidia kwa namna gani lakini pia
StarTimes ishirikiane na nyie ili kuona mnawezaje kurusha vipindi vitakavyo
elimisha umma juu ya ugonjwa huu wa moyo,” alisema Kanu.
Akitoa nasaha zake za
mwisho katika hafla iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam mwishoni mwa
wiki kabla ya kuondoka, Kanu alisema kuwa amefarijika sana kwa mapokezi
aliyoyapata toka siku ya kwanza uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam na mpaka
anaondoka nchini.
“Nimetembelea Uganda,
Kenya lakini mapokezi niliyoyapata Tanzania ni makubwa mno, na hii si mara ya
mwisho kuja Tanzania. Nimefurahi sana kwa ukarimu wenu nawaahidi kuja tena
nikipata fursa hiyo.“ Alihitimisha Kanu.
Mchezaji huyo nyota wa
zamani wa timu ya taifa ya Naijeria na vilabu mbalimbali vikubwa vya Ulaya kama
vile Ajax, Inter Milan na Arsenal ameitembelea Tanzania kama balozi wa
makampuni ya StarTimes barani Afrika kwa shughuli tofauti.
Katika uwepo wake nchini
Kanu ameshiriki katika shughuli kama vile;mahojiano mbalimbali na vituo vya
redio na luninga; ufunguzi wa duka la jipya la StarTimes lililopo katika jingo
la Mkuki Mall jijini Dar es Salaam; kutembelea taasisi ya moyo ya Jakaya Mrisho
Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili; kutoa misaada
mbalimbali kwa wanafunzi wenye ulemavu wa Shule ya Msingi Mbagala Majimatitu;
kutembelea na kushiriki mafunzo na vijana wa kituo cha Jakaya Mrisho Kikwete
jijini Dar es Salaam; kushiriki chakula cha jioni cha pamoja na wadau
mbalimbali wa michezo nchini pamoja na kualikwa kama mchambuzi katika mechi ya
soka la Bundesliga kati ya Bayern Munich na VFB Stuttgat katika kituo cha
luninga cha TBC2.
0 comments:
Post a Comment