.
Na
Raymond Mushumbusi MAELEZO
Jeshi
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata mtuhumiwa anayejulika kwa
jina la Wenceslaus Mtui(46) mkazi wa Makongo Juu kwa kosa la utapeli wa sh.
Milioni 90 .
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi kanda maaalum
ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro amesema wamefanikiwa kumkamata tapeli huyo
mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa Bw. Kelvin Nyerere(26) mkazi wa Msasani
ambaye alishawishiwa na kutapeliwa kwa kuuziwa madini bandia na mtuhumiwa huyo.
Kwa
mujibu wa kamanda Sirro, mtuhumiwa huyo alikamatwa mara baada ya kupata taarifa
kutoka kwa Nyerere aliyetapeliwa, askari walifika eneo la tukio na kumkamata
mtuhumiwa na kumfikisha kituo cha polisi
kwa mahojiano.
Aidha
baada ya kufanyika kwa upekuzi ofisini na nyumbani kwa mtuhumiwa, kulikutwa na
vitu vilivyodhaniwa kuwa ni madini, chuma cha kuchomea madini, mashine ya
kupimia madini, vifaa vya kubania madini (53), mashine ya kupimia madini,
nyaraka za kuwekea fedha kutoka Benki mbalimbali na hati za usajili wa
makampuni ambazo zilitiliwa shaka.Vielelezo vyote vilichukuliwa kwa uchunguzi.
Mtuhumiwa
huyo bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi upepelezi utakapokamilika atafikishwa
mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili za kufanya utapeli wa kuuza madini
bandia ambayo ni kinyume cha Sheria za nchi.
Jeshi
la Polisi linatoa onyo kwa watu wanaojifanya wafanyabiashara wa madini kuacha
mara moja tabia hiyo na wananchi wanaohitaji kununua madini wafike Ofisi za
Wakala wa Madini(TMAA) ili kuepukana na matapeli.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment