Na
Jacquiline Mrisho - MAELEZO
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Kinondoni amewataka walipa kodi na ushuru katika Manispaa hiyo
kudai stakabadhi za kielektroniki baada ya kufanya malipo ili kuziba mianya ya
upotevu wa mapato.
Rai
hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Aron
Kagurumjuli alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hii juu ya njia wanazozitumia
katika ukusanyaji wa ushuru wa Manispaa hiyo.
“Napenda
kuwasisitiza wananchi kuwa unapofanya malipo yoyote ya Manispaa lazima
uhakikishe unapewa stakabadhi ya kielekroniki na iwapo hutopewa, unaruhusiwa kutoa
taarifa kwa kupiga simu au kutuma ujumbe mfupi kwenda 0767643460 na utapatiwa
maelekezo ya nini cha kufanya”,alisema Kagurumjuli.
Kagurumjuli
ameongeza kuwa Ofisa yeyote atakayekaidi kutoa stakabadhi hizo atachukuliwa hatua
kali za kisheria kwani kukwepa kulipa mapato ni kurudisha nyuma uchumi wa nchi.
Aidha,
Mkurugenzi huyo ameyataja maeneo ambayo mwananchi anaweza kulipia kodi au
ushuru na kupata stakabadhi za kielekroniki ni Ofisi za Manispaa, Ofisi za
Kata, Benki ya CRDB pamoja na watumishi wa Manispaa waliopo katika shughuli
maalumu za ufuatiliaji wa kodi na ushuru.
Halmashauri
ya Manispaa ya Kinondoni ilianza kutumia mfumo wa kulipa kodi na ushuru kwa
njia ya kielekroniki mnamo mwaka 2013 , na mwaka 2015 ilipata tuzo ya
ukusanyaji bora wa mapato kwa njia hiyo kwa Tanzania na Afrika nzima.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment