Wednesday, June 29, 2016

UZINDUZI WA MPANGO WA KUJENGA TANZANIA YA VIWANDA



  Mkurugenzi Mtendaji wa Covenant Bank Sabetha Mwambenja, kwa Pamoja na Mkurugenzi wa Bega kwa Bega Microfinance Johakimu January, wakitia saini mkataba wa makubaliano ya Ushirikiano wa kazi kati ya Taasisi hizo ili kuwawezesha vijana kuanzisha makampuni na viwanda vidogo vidogo nchi nzima. Wanaoshuhudia ni Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( TAMISEMI), Suleiman Jaffo,  Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Manju Msambya, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Covenant Bank, Balozi. Salome Sijaona  hafla hiyo imefanyika jijini mwanza mwishoni mwa wiki hii.




003 & 004: Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Covenant Bank, Balozi. Salome Sijaona (wa pili kushoto) Pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Covenant Bank, Sabetha Mwambenja wakimkabidhi Mkataba wa Makubaliano Naibu waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Suleiman Jaffo  ili kuwawezesha vijana kuanzisha makampuni na viwanda vidogo vidogo nchi nzima.Pamoja nao katika picha kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Bega kwa Bega Microfinance Johakimu January.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu