UJENZI
WA HOSPITALI YA KISASA CHANIKA KUGHARIMU BILIONI 18
Na
Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Manispaa
ya Ilala kwa kushirikiana na Shirika la Misaada la Korea (KOICA) inatarajia kutumia kiasi cha shilingi
bilioni 18 kukamilisha Ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya kutolea huduma za
matibabu kwa mama na mtoto katika Kata ya Chanika,wilayani Ilala.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Afisa Habari wa Halmashauri ya Manispaa
ya Ilala, David Langa wakati akitoa ufafanuzi kuhusu maboresho yanayofanywa
katika Sekta ya Afya ndani ya Manispaa hiyo.
Amesema
hospitali hiyo itakamilika mwishoni mwa mwaka huu na kuongeza kuwa itakuwa na
vitanda 266 pamoja na mashine zote za upasuaji na matatibu ya magonjwa yote ya
wanawake na watoto.
“Ujenzi
wa Hospitali hii kubwa ya wanawake na watoto unaendelea, tutatumia shilingi
bilioni 18 kukamilisha kazi ya ujenzi na kuweka vifaa vya kisasa”,amesema
Langa.
Kwa
upande wake Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Meshach Simwela amesema
kuwa hospitali hiyo itakapokamilika itakuwa na vifaa vya kisasa pamoja na
madaktari bingwa kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili, Amana, Mnazi Mmoja pamoja
na hospitali nyingine za Serikali.
“Mpaka
sasa jumla ya waganga watano na wauguzi sita wameshapelekwa Korea kujifunza
namna ya kutoa huduma na jinsi ya kutumia vifaa vipya vitakavyoletwa mara baada
ya Hospitali hii kukamilika”, alisema Simwela.
Ameongeza
kuwa ujenzi huo unategemewa kukamilika mwaka huu na unategemewa kufunguliwa na
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli au Makamu
wa Rais Mhe.Mama Samia Suluhu kwa kuwa ni Hospitali ya kwanza nchini Tanzania
kuwa na hadhi kubwa kama hiyo.
0 comments:
Post a Comment