Meneja
Program
wa SATF Rogasian Massue, (kulia), akipeana mikono na meya wa Manispaa
ya Kinondoni Boniface Jacob, wakati akikabidhi madawati hayo
NA JANET JOSIAH.
MSTAHIKI
Meya wa Halimashauri ya Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob Leo Julai 22,
2016, amepokea msaada wa madawati 100 toka Shirika la Social Action Trust Fund (SATF)lenye
makazi yake Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
katika hafla hiyo fupi Meya Jacob alisema kwamba mpango ulipo kwa Manispaa hiyo
nikuhakikisha hadi mwezi Agosti mwaka huu, hakuna mwanafunzi atakayekaa chini
kutokana na kuwa na uwezo wa kuwatosheleza.
"
Nawashukuru sana nyie Shirika la SATF kwa msaada wenu huu kwetu Manispaa...
tunawaalika wadau wengine wa elimu kutuletea msaada mwingine wa madawati ili
yajae na mengine tuweke stoo akiba ili watoto watakapovunja wapewe mengine
maana ni watundu sana" alisema
Pamoja na
hilo Meya Jacob aliwataka wadau wengine wa elimu kujitokeza kutoa msaada
wa madawati kwa kuwa uhitaji wake bado upo.
Hata hivyo
alisema kuwa mpaka sasa wazabuni waliopewa kazi ya kutengeneza madawati zaidi
ya 16000 wanaendelea ili yaanze kugawiwa kwa shule za Manispaa hiyo haraka.
Mapema
Meneja Program wa SATF Rogasian Massue alisema kuwa watoa madawati yao 100 kama
mpango wao wa kusaidia wilaya mbalimbali ili vijana waweze kupata elimu na kuwa
wataalam mbalimbali.
Massue
alisema katika program ya kutoa msaada wa madawati 150 katika Halmashauri
ya Chato mkoani Geita, wakafuatilia Kinondoni jijini Dar es Salaam madawati
100.
Meneja
program huyo alisema sasa wanajiandaa kupeleka msaada Manispaa za Temeke na
Ilala za hapa jijini, wilaya ya Kankonko mkoani Kigoma na Kaliua
mkoani Tabora.
Meya Jacob
Meneja
Program wa SATF Rogasian Massue, (kushoto), akizungumza wakati wa makabidhiano hayo
0 comments:
Post a Comment