Friday, July 22, 2016

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura afanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mziki Tanzania Bw.John Kitime kuhusu kuboresha tasnia ya Mziki nchin

; Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime akisaini kitabu cha wageni alipowasili ofisini kwa Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura kuwasilisha taarifa ya mapendekezo ya kuboresha tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime akizungumza na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura ofisini kwa Naibu Waziri  wakati aki wasilisha taarifa ya mapendekezo ya kuboresha tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.

Afisa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Habibu Msammy  akichangia mada wakati wa majadaliano kati ya  na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime  kuhusu maboresho ya tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura akipokea  moja ya kazi ya muziki  wa dansi alizowahi kufanya Mzee Kitime baba wa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime(kulia),  wa pili kushoto ni Afisa Utamaduni  kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Habibu Msammy  na kushoto katibu wa Naibu Waziri Bi. Anna Nkinda  leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.

( Picha zote na Shamimu Nyaki WHUSM)

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu