Monday, July 18, 2016

Na Raymond Mushumbusi WHUSM

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye ameahidi kupambana na wale wote wanaojihusisha na wizi wa kazi za wasanii na kuzisambaza kinyume cha sheria.

Mhe. Nape Nnauye ametoa ahadi hiyo mbele ya wasanii na wadau wa sanaa wakati akizundua filamu ya Sikitu na kuahidi kutochoka kupambana katika vita dhidi ya wezi wa kazi za wasanii wa filamu na sanaa kwa ujumla.

“Nataka niwahakikishie wasanii na watengeneza filamu Tanzania kazi hii nimeianza na nitaendelea nayo na hatutoshindwa tutashinda na nawaonya wanaofanya kazi ya kuiba kazi za wasanii waache mara moja” alisema Mhe. Nnauye.

Mhe. Nnauye ameongeza kuwa Serikali itaendelea kujenga misingi mizuri kwa wasanii na tasnia ya filamu Tanzania na kuhakikisha wasanii na watayarishaji wanapata mitaji itakayowawezesha  kuzalisha filamu bora na kupata masoko mazuri.

Aidha amewaomba wadau wa sanaa na filamu kwa ujumla kukaa na Serikali na kuangalia namna bora ya kurasimisha vibanda vinavyoonesha filamu za kitanzania kuwa kumbi maalum kwa ajili ya kuonesha filamu hizo ili kuongeza soko la filamu hizo kupitia kumbi hizo.

Kwa upande wake katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo amewapongeza watayarishaji wa filamu hiyo kwa kuzingatia maadili na wazidi kutengeneza filamu zenye ubora zaidi ili kukuza tasnia ya filamu nchini.

Filamu ya Sikitu imetayarishwa na kutengenezwa na  Kajala Entertainment na imehusisha wasanii wengi wenye uwezo mkubwa akiwemo Taiya, Mutrah, Jada, Asha Boko, Hemed Suleimani, kajala Masanja, Amir Athuman ‘King Majuto’ na wengine wengi, imeandikwa na kuongozwa na Leah Richard Mwendamseke na itaoneshwa katika kumbi za sinema kwa muda wa siku saba kabla ya kuingia sokoni.

Mwish
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu