Sunday, October 30, 2016

WALIPEWA WIKI MOJA KUTOA MAONI, BADO WANADAI MUDA ZAIDI.

MWENYEKITI KAMATI ASEMA KWA MIAKA MINGI WAMEKUWA WAKIKWAMISHA MUSWAADA HUO.

Na Mwandishi Wetu Dodoma

Wadau wa habari nchini wameendelea kukacha kuudhuria kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na hata kutoa maoni yao licha ya kupewa barua za mwaliko na kuongezewa siku kumi za ziada kuwasilisha maoni yao kuhusu Muswaada wa Sheria ya Huduma za Habari.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakati akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati Huyo Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa wao kama Kamati wanaendelea na kazi ya kisheria ya kutunga Sheria.

Ameongeza kuwa wadau walikuja kwa mara kwanza mbele ya kamati na kupewa nafasi ya kutoa maoni yao kuhusu Muswaada lakini walisema muda mchache wanahitaji muda zaidi  wa kuusoma Muswaada na kuto amaoni yao.

Mhe. Serukamba amesisitiza kuwa hii imekuwa tabia ya wadau walio wengi kila Muswaada huu unapoletwa Bungeni wamekuwa wakisema hawako tayari na kuomba utolewe Bungeni.

“Kwa miaka 23 Serikali imekuwa ikiwasikiliza wadau mpaka mwaka jana Muswada uliletwa Bunge lakini wakataa na kutaka urudishwe na kwa sasa wamerudia tena na sisis kama Kamati tutaendelea na kazi yetu ya kutunga Sheria kwa kuzingatia maoni yaliyotumwa” alisema Mhe. Serukamba.

Aidha, kwa kuzingatia Kanuni za Bunge mara baada ya Muswaada kusomwa kwa mara ya kwanza ni jukumu la wadau kuusoma Muswaada kwani unakuwa wazi kwa umma kwa ajili ya kuusoma na kutoa maoni yao ili kuuboresha Muswaada husika.

Mhe. Serukamba amewataja wadau walikokiri kupata barua ya mwaliko lakini bado hawakuweza kuwasilisha maoni yao wala kufika kwenye  kamati yake kama walivyoomba kuongezewa muda wa kutoa maoni na bado wanasema Muswaada unahitaji muda zaidi ili waweze kuusomwa Muswaada na kutoa maoni yao.


Amewataja wadau hao kuwa ni, Pili Mtambalike, Legal and Huma Rights Centre, Union of Tanzania Press Club, na Media Council of Tanzania (MCT).

Baadhi ya wadau mmoja mmoja na kwa vikundi wamewasiliasha maoni yao katika Kamati hiyo kwa njia ya barua pepe wakiwemao Chama cha wanasheria wa Tanganyika (Tanganyika Law Society (TLS)).

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imekutana leo Oktoba 29 kupokea maoni ya wadau wa habari nchini ili kuendelea na maboresho ya Muswada huo kabla ya kupelekwa kujadiliwa  Bungeni.

MWISHO.
WAZIRI WA HABAR

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu