Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akimfariji mama Margareth Sitta, mke
wa marehemu Samwel Sitta, wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa marehemu
Sitta kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Novemba 11,
2016.
NA
K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID
VILIO
na majonzi vilitawala viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam wakati Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akiongoza watanzania
kuuaga mwili wa Marehemu Samwel Sitta, spika wa bunge la 9 la serikali ya awamu
ya nne.
Marehemu
Sitta aliyejulikana sana kwa jina la “Mzee wa Kasi na Viwango” alifariki dunia
mapema wiki hii mjini Munich nchini Ujerumani alikokuwa akipatiwa matibabu ya
Tezi Dume.
Mwili
wa marehemu Sitta ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za serikali na
chama chake cha CCM kwa takriban miaka 49, ulisafirishwa kwenda mjini Dodoma
ambako ibada maalum imeandaliwa ambapo mwili wake utaagwa kwenye jumba la bunge
mjini Dodoma kabla ya kusafirishwa kwenda kijijini kwake wilayani Urambo mkoani
Tabora ambako atazikwa Jumamosi.
Marehemu
Sitta, ambaye pia alijulikana kama “Chuma cha Pua” kutokana na msimamo wake
mkali katika kusimamia masuala yenye maslahi na Taifa, atakumbukwa kwa mambo
mengi lakini kubwa zaidi ni pale alipokuwa spika wa bunge la 9 ambalo kwa
watanzania wanaliona kama bunge la Kihistoria ambapo alilifanya liwe na “Meno”
na kujizolea umaarufu mkubwa kwa watanzania wa kawaida kutokana na jinsi
alivyoliongoza katika kutekeleza wajibu wake wa kuisimamia serikali.
Rais Magufuli akitoa heshima zake za mwisho mbele ya mwili wa marehemu Samwel Sitta
Rais mstaafu wa serikali ya awamu ya
tatu, Benjamin Mkapa, na Mama Anna Mkapa wakitoa heshima zao za mwisho
mbele ya mwili wa marehemu Samwel Sitta
Rais mstaafu wa serikali ya awamu ya
nne, Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete, wakitoa heshima zao za
mwisho mbele ya mwili wa marehemu Samwel Sitta
Rais Magufuli akimpa pole mtoto wa marehemu, Benjamin Sitta
0 comments:
Post a Comment