Na
Mwandishi Wetu
Serikali
kupitia Wizara ya Ujezi Uchukuzi na Mawasilano imebariki uzinduzi wa
televisheni mpya ya kidigitali kutoka kampuni ya Startimes Tanzania.
Akizungumza
katika uzinduzi huo kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.
Prof Makame Mbarawa, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Maria Sasabo amesema
Serikali imefarijika sana na ubunifu kutoka kwa kampuni ya StarTime Tanzania
kwa kuanzisha televisheni ya kidigitali isiyotumia kinga’muzi kupata matangazo
ya channeli mbalimbali.
“Hii
ni fursa kwa watanzania kujipatia televesheni hizi ambazo ziko katika teknolojia
ya hali juu sana ambazo zitasaidia Tanzania kuingia katika ulimwengu mpya wa
mapinduzi ya sekta ya Habari na Mawasiliano” alisema Bibi. Maria.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa StarTimes Tanzania Bw. Leo Liao amesema kuwa
StarTimes imelazimika kutoa televisheni hizo za kisasa ili kuendana na ukuaji
wa teknolojia ambapo wateja wataweza vipindi vinavyoenda na wakati katika ubora
wa hali ya juu.
“Tutahakikisha
tunawapa wateja wetu vipindi vyenye ubora na muonekano mzuri ambao wataufurahia
ulimwengu wa Digitali unaoendelea kubadilika kila kukicha duniani” alisistiza
Bw. Liao.
Ameongeza
kuwa televisheni hizo zimetengenezwa katika ubora unaotakiwa na ni rafiki kwa
mazingira na zimezingatia matumizi madogo ya umeme na zinapatikana kwa bei
nafuu ukilinganisha na televisheni kutoka makampuni mengine.
Televisheni
hizo za kidigitali zinaonesha zaidi ya channeli 100 za kitaifa na kimataifa
kuanzia habari, muziki, michezo, sinema, thamthilia,katuni, filamu na vipindi
vya Dini.
MWISHO.
Mkurugenzi Mkuu wa StarTimes Tanzania Bw.
Leo Liao(kushoto) akikabidhi zawadi ya moja ya televisheni za kidigitali yenye
upana wa inchi 40 kwa mshindi wa televisheni hiyo Bw.John Paul wakati wa hafla ya uzinduzi wa televisheni
hizo uliofanyika Novemba 16,2016 Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment