Na Daudi Manongi-MAELEZO.
SHIRIKA la Maendeleo
ya Petroli Nchini (TPDC) limeipatia shilingi milioni 10 Ofisi ya Serikali ya
Mtaa wa mji Mpya iliyopo Pugu Majohe Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kwa
ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Serikali hiyo.
Akizungumza katika hafla
hiyo leo Jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Shirikahilo, Mhandisi Kapulya Musomba
alisema wakazi wa Pugu-Majohe wameamua kutoa fedha hizo kutokana na wakazi wa
eneo hilo kupitiwa na bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
“TPDC hatuwezi kulinda bomba hili la Gesi
kila mahali linapopita, wadau hawa wamekuwa ni sehemu ya kulinda bomba hili
wanalinda pia uchumi wa nchi kwa sababu gesi hii pia inatumika kuzalisha umeme
wa viwanda” Alisema Musomba.
Aidha Mhandisi Musomba ametoa wito kwa wananchi wa Pugu Majohe kuacha kuchimba mchanga karibu na bomba hilo kwani kwa kufanya hivyo watakuwa
wanaharibu miundombinu ya bomba hilo.
Kwa upande wake Kaimu
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas ameishukuru TPDC kwa kuwawezesha
kupata kiasi hicho kwani kitawasaidia katika ujenzi wa Ofisi hizo na pia katika
maendeleo ya Pugu Majohe na kuwaomba kuendelea kusaidia katika maeneo tofauti
ya Wilaya ya Ilala.
Nae Mwenyekiti wa
Serikali ya Mtaa mji Mpya-Majohe Bw.Geofrey Chacha amesema kuwa wamejiskia
faraja sana kwa kupata msaada huo kutoka TPDC kwani utaweza kusaidia kumalizia
ujenzi wa Ofisi zao.
Mchango huu umetupa
nguvu katika kuwahamasisha wananchi katika eneo hili kuweza kuwa walinzi wazuri
wa miundombinu hii ambayo inagusa maslahi ya Taifa letu” alisema Chacha.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa shilingi milioni 10 toka kwa Shirika la Petroli Nchini(TPDC) kwa ajili ya Ulinzi mzuri wa Bomba la Gesi linalopita jirani yao.
Kaimu Mkurugenzi Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Mhandisi Kapulya Musomba akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Serikali ya Mtaa,katikati ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas. Wakazi wa Majohe ni wadau wa Bomba la Gesi linalotokea Mtwara hadi Dar es Salaam
0 comments:
Post a Comment