Monday, December 19, 2016

TPDC YATOA SHILIONI MILIONI 10 WAKAZI WA PUGU-MAJOHE.



Na Daudi Manongi-MAELEZO.
SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) limeipatia shilingi milioni 10 Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa mji Mpya iliyopo Pugu Majohe Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Serikali hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo leo Jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Shirikahilo, Mhandisi Kapulya Musomba alisema wakazi wa Pugu-Majohe wameamua kutoa fedha hizo kutokana na wakazi wa eneo hilo kupitiwa na bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
“TPDC hatuwezi kulinda bomba hili la Gesi kila mahali linapopita, wadau hawa wamekuwa ni sehemu ya kulinda bomba hili wanalinda pia uchumi wa nchi kwa sababu gesi hii pia inatumika kuzalisha umeme wa viwanda” Alisema Musomba.
Aidha  Mhandisi  Musomba  ametoa wito kwa wananchi wa Pugu Majohe  kuacha kuchimba  mchanga  karibu  na  bomba hilo kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wanaharibu miundombinu ya bomba hilo.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas ameishukuru TPDC kwa kuwawezesha kupata kiasi hicho kwani kitawasaidia katika ujenzi wa Ofisi hizo na pia katika maendeleo ya Pugu Majohe na kuwaomba kuendelea kusaidia katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Ilala.
Nae Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa mji Mpya-Majohe Bw.Geofrey Chacha amesema kuwa wamejiskia faraja sana kwa kupata msaada huo kutoka TPDC kwani utaweza kusaidia kumalizia ujenzi wa Ofisi zao.
Mchango huu umetupa nguvu katika kuwahamasisha wananchi katika eneo hili kuweza kuwa walinzi wazuri wa miundombinu hii ambayo inagusa maslahi ya Taifa letu” alisema Chacha.


Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa shilingi milioni 10 toka kwa Shirika la Petroli Nchini(TPDC) kwa ajili ya Ulinzi mzuri wa Bomba la Gesi linalopita jirani yao.

Kaimu Mkurugenzi Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Mhandisi Kapulya Musomba akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Serikali ya Mtaa,katikati ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas. Wakazi wa Majohe ni wadau wa Bomba la Gesi linalotokea Mtwara hadi Dar es Salaam

: Wakazi wa Pugu Majohe  wakifurahi kupatiwa hundi ya shilingi milioni 10 kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Serikali ya Mtaa . Wakazi wa Majohe ni wadau wa Bomba la Gesi linalotokea mtwara hadi Dar es Salaam.
Picha na Daudi Manongi-MAELEZO.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu