Kesho tarehe 19/01/2017 Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Nnape Nnauye atakutana na wadau mbalimbali
wa sekta ya filamu. Mkutano wa Mheshimiwa Nnape na wadau hao utafanyika kwenye
ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO kuanzia saa nne (4) asubuhi.
Lengo la mkutano ni kujadili
changamoto mbalimbali zinazohusu sekta ya filamu na kuzitafutia ufumbuzi wa
kudumu kwa ajili ya maendeleo ya sekta husika.
Natanguliza shukran za dhati kwa
ushirikiano wako.
imetolewa na;
OFISI YA UHUSIANO NA MAWASILIANO
BODI YA FILAMU TANZANIA
0 comments:
Post a Comment