Benchi la Timu ya Simba likifuatilia mchezo wao wa Pili wa Kombe la
Mapinduzi Cup ikicheza na Timu ya KVZ, mchezo uliofanyika katika uwanja
wa Amaan. Timu ya Simba imeshinda bao moja bila, ikiongoza katika kundi
lake hilo kwa kuwa na pointi 6. kwa kushinda michezo yake miwili.
ikifuatiwa na Timu za Jangombe Boys, Taifa ya Jangombe na URA zikiwa na
pointi tatu kila moja baada ya kucheza michezo miwili kila moja katika
kundi lao hilo.
Kocha wa Timu ya Simba akiwa uwanjani akifuatilia wachezaji wake wakati
wa mchezo wao wa Kombe la Mapinduzi Cup, ikicheza na Timu ya KVZ, katika
mchezo huo timu ya Simba iomeshinda bao 1--0.
0 comments:
Post a Comment