|
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan amesema mazingira yanatuadhibu kutokana na uharibifu unaofanywa
na mwanadamu.
Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa ukaguzi wa mradi wa
ujenzi wa ukuta wa bahari katika eneo la Kigamboni na Ocean Road jijini Dar es
Salaam.
Akihutubia wananchi waliojitokeza katika Chuo Cha Kumbukumbu
ya Mwalimu Nyerere ambacho ukuta wenye urefu wa mita 500 unajengwa sambamba na
sehemu za kupumzikia, Makamu wa Rais alisema “ tumeharibu mazingira na mazingira yanatupa adhabu lazima sasa turudi
wote tuwe rafiki wa mazingira, turekebishe pale tulipoharibu, turekebishe pale
tulipokosea ili mazingira yarudi tena yawe rafiki yetu”
Makamu wa Rais alisema kuwa uamuzi wa kufanya miradi ya
kujenga ukuta wa bahari ni kuzuia bahari isiendelee kula ardhi.
Makamu wa Rais alisema pamoja na kujenga Ukuta huo unategemewa
kudumu kwa miaka zaidi ya 70 , pia wamejenga mitaro kwa ajili ya kuzuia maji ya
mvua yasilete madhara katika maeneo ya Ilala na Temeke.
Wakati huo huo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesema uharibifu wa mazingira ni
janga la kitaifa hivyo alimpongeza Makamu wa Rais kwa kupaza sauti katika suala
zima la utunzaji wa mazingira.
Vilevile Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda
amesema mkoa wa Dar es salaam utaendelea na kampeni ya kupanda miti
inayojulikana kama Mti Wangu kwani kampeni hiyo ilikuwa moja ya maelekezo ya
Makamu wa Rais.
|
: Ujenzi wa Ukuta wa bahari katika eneo la umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
|
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiongozana na Meneja wa Mradi na Miundo Mbinu wa UNOPS Bw. Bernard
Odhuno wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari
Kigamboni wenye urefu wa mita 500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
|
|
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiongozana na Meneja wa Mradi na Miundo Mbinu wa UNOPS Bw. Bernard
Odhuno wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari
Kigamboni wenye urefu wa mita 500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
|
|
Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January
Makamba akifafanua jambo mbele ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkuu wa mkoa wa Dar es
Salaam Mhe. Paul Makonda wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa
ukuta wa bahari Ocean Road. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
|
|
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiwa ameketi kwenye moja ya sehemu za kupumzikia pamoja na
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.January
Makamba(kulia) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa dar es Salaam Mhe. Paul
Makonda wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa ukuta
wa
bahari Kigamboni wenye urefu wa mita 500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa
Rais)
|
0 comments:
Post a Comment