Saturday, January 20, 2018

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakifurahia jambo baada ya Mhe. Rais kuongea na watumishi wa Wizara hiyo kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Karume, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama a Taifa Dkt. Modestus Kipilimba na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiagana na  Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masshariki  baada ya kuongea nao kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu